KINANA NA UJUMBE WAKE WAWASILI ZANZIBAR KUZINDUA KAMPENI ZA CCM LEO




Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (watano kulia) na ujumbe wake wa viongozi waandamizi kutoka makao makuu ya CCM, wakiwa kwenye chumba cha nahodha walipokuwa wakisafiri kwa boti ya mwendokasi kutoka Dar es Salaam, kwenda Zanzibar kwa ajili ya kushiriki uzinduzi wa kampeni za CCM, uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Dimani, leo. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara, Rodrick Mpogolo

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akihoji moja ya kifaa cha kuongozea boti ya mwendo kasi kinavyofanya kazi.

Karibu Zanzibar 

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Rodrick Mpogolo akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mjini Magharibi, Aziza Mapuri baada ya msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana kuwasili Bandari ya Zanzibar leo 
"NAAM TUMEWASILI KWA MUDA SAHIHI" Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimwambia Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Zanzibar Vuai Ali Vuai baada ya kuwasili Bandari ya Zanzibar leo 
Katibu Mwenezi wa CCM, Humphrey Polepole (kushoto) baada ya kuwasili Bandari ya Zanzibar 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo (kushoto) alipowasili Bandari ya Zanzibar leo

Humphrey Polepole akilakiwa baada ya msafara wa Kinana kuwasili Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui leo 
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mjini Magharibi Aziza Mapiri akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuhusu hali ya kampeni za uchaguzi mdogo wa Ubunge jimbo la Dimani walipokuwa katika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar leo 


Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana na msafara wake wakitazama eneo alilouliwa muasisi wa Mapinduzi ya zanzibar, Hayati Abeid Amani Karume katika Ofisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar, leo





Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiagwa na viongozi wakati akitoka Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar kwenda kwenye mapumziko kabla ya kwenda kwenye uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo jimbo la Dimani leo jioni. Picha zote na Bashir Nkoromo

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.