Eribariki Kingu:Naomba niwe wa kwanza kufukuzwa CCM kwa kumpinga Rc Makonda

Nilisema Nitanyamaza lakini Nimeshindwa. Nimethibitisha bila mashaka Clouds kuvamiwa na Rc akiwa na ulinzi na askari wenye silaha mpaka kwenye matangazo.

Najua hofu mliyonayo watanzania juu ya huyu Rc.

Ikiwa mamlaka zitaendelea kufumbia macho.Mimi Elibariki Immanuel Kingu mbunge wa CCM nitakuwa wa kwanza kufukuzwa CCM kama kupinga matendo maovu ya Rc huyu itaonekana ni usaliti kwa nchi.

Haiwezekani Rais wetu atukanwe kila kona kwa matendo ya mtu huyu.

Wana CCM ukimya wetu kwenye hili halikubaliki.

Magufuli juzi ametuliza Dodoma kwa kuongea kwa hisia.Idara za usalama kweli mmeamua kuacha tutukanwe?

Naomba sasa niweke kumbukumbu sawa najua mnamchafua kila anayempinga RC huyu kwa matendo yake ambayo yanakiuka utawala bora.

Naomba niwe wa kwanza kufukuzwa CCM kwa kumpinga Rc Makonda

Elibariki Immanuel Kingu
Mbunge.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.