Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Coca Cola, Nakala
Hettiarachch (Kulia ) akiwaeleza wanahabari jijini Dar es Salaam leo, kuhusu
mashindano ya Dasani Marathon yanayotarajia kuanza Mei 14, mwaka huu jijini Dar
es Salaam na Mgeni rasmi atakuwa Mwanariadha mstaafu wa Kimataifa, Juma Ikangaa.
Kushoto ni Rais wa Dar running club , Goodluck Elvis. (PICHA NA DALILA SHARIF).
Abraham Ntamabara
MWANARIADHA wa Mstaafu wa Kimataifa
Juma Ikangaa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mashindano ya riadha ya Dasani
Marathon yatakayo fanyika mei 14 mwaka huu jijini Dar es salaam.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es
Salaam na Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Coca-cola Nalaka Hetterachchi wakati
akizungumza na vyombo vya habari, alisema dhamira ya mashindano hayo ni
kuendeleza mchezo Wa riadha pamoja na kukuza uchumi nchini.
“Coca-cola imedhamini mbio hizi,
washiriki watakimbia katika mbio za kilomita 10 na 21, zitashirikisha
wakimbiaji zaidi ya 1000 ambapo zawadi mbali mbali zitatolewa kwa washindi, mshindi
wa kwanza atajinyakulia medali,” alisema Hetterachchi.
Mwanariadha Mstaafu Juma Ikangaa
alisema ili mshiriki aweze kupata ushindi katika mashindano hayo ni lazima
ujiandae, hivyo amewaomba wadau mbali mbali wajitokeze ili kuweza kushinda
medali hizo.
Juma alisema kuwa, angefurahi kuona rekodi ya kimataifa ya watu maarufu
katika mbio hizo ili kuleta mabadiliko
katika tasnia ya michezo ulimwenguni kote pamoja na kutoa hamasa kwa
Vijana.
Kwa upande wa Rais wa Dar Running club Goodluck Elvis alibainisha
kuwa mbio hizo zilianza miaka mitatu iliyopita na zimekuwa zikipata umaarufu.
Alieleza kwamba wamejiandaa vya kutosha ili kuhakikisha usalama unakuwepo siku
ya mashindano.
Aliwataka wananchi kujitokeza
kuchukua fomu za kujisajili ili kushiriki katika mashindano hayo. Alitaja vituo
vya kuchukulia fomu hizo kuwa ni Colosseum Gym masaki, shoppers supermarket mikocheni
na mlimani city Mall.
Mwisho
Comments