PLUIJM NA SINGIDA UNITED YAKE HAO MDOGOMDOGO NDANI YA MWANZA



Timu ya soka ya Singida United ya mkoani Singida ambayo imepanda daraja hivi karibuni na itashiriki michuano ya Ligi Kuu Bara msimu ujao, ipo mbioni kuhamishia makazi yake kwa muda jijini Mwanza.

Hatua hiyo imekuja baada ya kocha mkuu wa timu hiyo, raia wa Uholanzi,  Hans van Der Pluijm kuutaka uongozi wa klabu hiyo kufanya hivyo kutokana na hivi sasa kutokuwa na uwanja wa kufanyia mazoezi baada ya ule wa Namfua ambao ndio inaoutumia kuwa kwenye matengenezo.

Mwenyekiti wa Singida United, Yusuph Mwandami, amesema kuwa baada ya mapendekezo hayo ya Pliujm, kwa pamoja walikubaliana na ushauri huo, hivyo muda wowote mambo yatakapokuwa sawa, timu hiyo itaenda kukaa kwa muda jijini Mwanza.

“Hata hivyo, pindi uwanja wetu wa Namfua utakapokuwa tayari, basi timu itarudi Singida kuendelea na maandalizi yake kwa ajili ya ligi kuu.

“Niwaombe tu wapenzi na mashabiki wetu, hususan wakazi wa mkoani Singida, kuwa wavumilivu katika kipindi chote ambacho timu yao itakapokuwa Mwanza,” alisema Mwandami.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.