Abraham Ntambara
BENKI ya TIB Corporate imesema tangu
kuingia makubaliano na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mei 16 mwaka huu ya
kukusanya kodi kwa masaa 24 kumekuwa na mwamko mkubwa wa wananchi kujitokeza
kulipa kupitia tawi lao dogo la Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) lililopo
ndani ya Bandari.
Akizungumza na waandishi wa habari
jana jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa TIB
aliwataka wanchi kuendelea kulipia kodi kupitia benki hiyo. Alisema hilo
linaenda sambamba na agizo alilotoa Rais John Magufuli kuzitaka taasisi husika
katika bandari kutoa huduma siku zote kwa masaa 24.
“Benki ya TIB Corporate inawawezesha
wananchi wote kulipia kodi za aina mbalimbali pamoja na tozo zote za bandari.
Benki imejipanga vyema ili kuhakikisha huduma hii inaleta ufanisi na urahisi
zaidi kwa mlipaji,” alisema Nyabundege.
Aidha alibainisha kuwa hivi karibuni
benki hiyo iliingia mkataba na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuunganisha
mfumo wa malipo ya kodi ujulikanao kama TAXBANK.
Nyabundege alifafanua kwamba kupitia
mfumo huo, mlipa kodi akilipia katika tawi lolote la benki, taarifa zake
zinaonekana mara moja katika mtandao wa TRA hivyo kumuwezesha mlipa kodi
kuendelea na taratibu zingine kwa haraka zaidi.
Alisema benki ya TIB Corperate ndiyo
yenye dhamana ya kusimamia sehemu kubwa ya akaunti za mamlaka ya Bandari TPA
hivyo mwananchi anapolipia tozo yoyote ya bandari taarifa zake taarifa zake
zitaonekana kwenye mtandao wa TPA ambazo zitarahisisha na kuwezesha kuendelea
na taratibu zingine.
Aidha alisema wapo katika mpango
mkakati wa kujitanua na kutoa huduma kama hiyo kwenye bandari nyingine nchini
ambapo alibainisha kuwa wanatarajia kwenda kwenye bandari za Mtwara na Tanga
kwa ajili ya ukusanyaji wa kodi.
Aliongeza kuwa ni malengo yao pia
kuweka ofisi zao nje ya nchi kama Kongo, Zambia na Uganda ambazo zitakuwa
zikitoa huduma hiyo na kuahakikisha mapato ya nchi yanakusanywa pasipo kuleta
usumbufu kwa mlipaji.
Aliwataka wananchi wanaohitaji huduma
hiyo kutokuwa na hofu kwani wanaweza kufika wakati wowote na kuhudumiwa tofauti
na awali ambapo ofisi zilikuwa zikifungwa saa 12 jioni.
mwisho
Comments