RAIS John Magufuli amepiga marufuku wanafunzi wanaopata mimba kuruhusiwa kwendelea na masomo.
Agizo hilo amelitoa leo alipokuwa akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Barabara ya Msata-Bagamoyo mkoani Pwani.
Rais amesema kuwa katika katika kipindi cha urais wake hatoruhusu wanafunzi wenye mimba na waliozaa kuendelea na masomo akihofia hali hiyo inaweza kuwahamasisha wanafunzi wengine kupata mimba.
Alizitaka NGO'S zinazohamasisha jambo hilo haziitakii mema Tanzania, na endapo wanataka mambo hayo yaendelee basi waanzishe shule zao za kuwafundisha wanafunzi waliozaa.
Pia aliimpongeza Mke wa Rais Mstaafu, Mama Salma Kikwete kwa msimamo wake akiwa bungeni Dodoma kupinga wanafunzi wanaopata mimba kuendelea na masomo.
Rais Magufuli alisema kwamba, hawezi kutumia sh. bil 18 zinazotengwa kila mwezi kugharamia wanafunzi, zitumike kuwagharamia wenye mimba ambao wamejitakia kwa kuendekeza ngono. Wanafunzi ambao hawataendelea kuendelea na masomo wakiwa na mimba ni kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha sita.
Agizo hilo amelitoa leo alipokuwa akihutubia wakati wa hafla ya uzinduzi wa Barabara ya Msata-Bagamoyo mkoani Pwani.
Rais amesema kuwa katika katika kipindi cha urais wake hatoruhusu wanafunzi wenye mimba na waliozaa kuendelea na masomo akihofia hali hiyo inaweza kuwahamasisha wanafunzi wengine kupata mimba.
Alizitaka NGO'S zinazohamasisha jambo hilo haziitakii mema Tanzania, na endapo wanataka mambo hayo yaendelee basi waanzishe shule zao za kuwafundisha wanafunzi waliozaa.
Pia aliimpongeza Mke wa Rais Mstaafu, Mama Salma Kikwete kwa msimamo wake akiwa bungeni Dodoma kupinga wanafunzi wanaopata mimba kuendelea na masomo.
Rais Magufuli alisema kwamba, hawezi kutumia sh. bil 18 zinazotengwa kila mwezi kugharamia wanafunzi, zitumike kuwagharamia wenye mimba ambao wamejitakia kwa kuendekeza ngono. Wanafunzi ambao hawataendelea kuendelea na masomo wakiwa na mimba ni kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha sita.
Comments