MSUVA SAFARI YA KUONDOKA YANGA IMEIVA SASA NI TIMU TATU KUTOKA NCHI TATU


Timu tatu kutoka katika nchi tatu, sasa zinataka kumsajili kiungo wa pembeni wa Yanga, Simon Msuva.

Timu hizo zinatokea katika nchi za Morocco, Misri na Afrika Kusini na Msuva amethibitisha hilo.

Akizungumza na SALEHJEMBE, amesema tayari ofa hizo zimetua mezani Yanga na yeye ana taarifa.

“Nina tarifa nao na klabu inajua, hivyo ni suala la makubaliano kati yao na klabu na kati yao na mimi,” alisema.

Alipoulizwa katika ofa hizo tatu angependelea kwenda wapi kati ya Morocco, Misri au Afrika Kusini, alijibu.

“Hapa ni suala la ofa tu, nitaangalia timu na maslahi. Hivyo ni suala la kusubiri tu,” alisema.

Msuva amemaliza Ligi Kuu Bara akiwa na mabao 14 sawa na Abdulrahman Mussa na wote mwisho wameibuka wafungaji bora.


Kijana huyo wa Kitanzania amekuwa akionyesha juhudi kubwa katika misimu minne mfululizo sasa hali inayoonyesha kuzivutia timu kadhaa za nje ya Tanzania.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.