YANGA YAWAPIGA CHENGA WACHAWI WA SIMBA AIRPORT DAR.

TIMU ya Yanga imetua Uwanja wa Ndege wa zamani Dar es Salaam kwa kuwapiga chenga ya mwili 'wachawi' wa Simba.

Yanga waliowasili saa 12:30 jana jioni kwa Ndege ya kukodi kutoka Pemba, wakiongozwa na Mama Fatma Karume walikwepa kupita mlango wa kawaida wa abiria ambako inadaiwa 'wachawi' wa Simba waliojichanganya na mashabiki walikuwa wanawasubiri ili wawatende.

Kwa mujibu wa Mmoja wa wafanyakazi wa Ndege za kukodi aliyekuwepo uwanjani, alishuhudia Timu hiyo ikikwepa mtego huo kwa kupanda kwenye coaster iliyoingizwa ndani mapema ikitoka Aiport kupitia geti la Polisi na kutokomea town.

Kitendo hicho kiliwaacha hoi 'wachawi. hao pamoja na Mashabiki wa Yanga waliobaki kulikodolea macho gari hilo likitokomea.

Shuhuda huyo anasema kuwa 'wachawi' wa Simba waliokuwepo hapo walionekana kupigwa na mshangao huku wakiwa wameshika mikono kichwani na kusikika wakisema "Ayaa wamepitia kule sasa tumekwisha."

Alisema kuwa makomandoo wa Yanga walikuwepo uwanjani hapo tangu mapema kuweka usalama kwa timu yao ili isidhurike kwa lolote ambapo walionekana kuwapiga mkwara mzito waliowahisi kuwa 'Wachawi' wa Simba kwa kuwaamuru kuondoka na kuacha kukaribia lango la kutokea abiria.

Timu hiyo inayocheza na Simba  kwenye Ngao ya Jamii ilipokelewa Airport na Katibu Mkuu wa Klabu ya Yanga, Boniface Mkwasa na Shadrack  Nsajigwa.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.