NDEGE KUBWA YA ABIRIA YA EMIRATE KUTUA NCHINI YAIPANDISHA TANZANIA KATIKA UTOAJI WA UTOAJI HUDUMA YA USAFIRI WA ANGA
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Mamlaka
ya Usafiri wa Anga (TCAA) imesema kuwa kutua kwa Ndege kubwa ya
‘gorofa’ A380 ya Fly Emirates imedhihirisha kuwa uwanja wa Kimataifa wa
ndege wa Mwalimu Julius K Nyerere na vyombo vyake kuwa madhubuti
katika usafiri wa anga.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka
hiyo, Hamza Johari amesema kuwa ndege hiyo licha kupata udhuru wa
kushindwa kutua katika uwanja wa ndege wa Mauritius kumeipa heshima nchi
katika kuwa na viwango katika utaoaji huduma ya usafiri wa anga.
Amesema
kuwa Rubani wa ndege A380 ya Fly Emirates alifanya busara ya kuamua
baada ya kuona hali ya hewa ya Mauritius kutokuwa nzuri na kuamua kutua
kwenye Uwanja wetu wa kimataifa wa Mwalimu Julius K Nyerere na
kuamini kuwa atatua bila wasiwasi.
Johari
amesema kufuatia kutua kwa ndege hiyo kubwa nchi imeweza kupata mapato
katika huduma mbalimbali za kijamii kutokana na abiria waliokuwa katika
ndege hiyo zaidi ya watu 500 ambao wote walilala katika hoteli zilizopo
nchini.
Amesema
kuwa ndege hiyo kubwa ya abiria duniani ndio mara ya kwanza kutua
katika uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius K. Nyerere hivyo inaonyesha
kujizatiti katika utoaji katika utoaji wa huduma ya usafiri wa anga.
Ndege
hiyo imetua Aprili 24 katika uwanja wa Ndege Mwalimu Julius Nyerere
ikitokea Dubai ambaye ilishindwa kutua mara tatu katika uwanja wa
Mauritius na kuja kutua Tanzania
Mkurugenzi
Mkuu huyo amesema kuwa wamekuwa na asilimia 64 kutoka 37 kwa viwango
vilivyowekwa na Shirika la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) hivyo tuzo
yake itatolewa na Rais wa shirika hilo kwa kumkabidhi Rais Dk.John Pombe
Magufuli na mawasilino yanafanyika yanafanyika ujio wa Rais wa ICAO.
Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), Hamza Johari akizungumza na
waandishi habari kuhusiana na kutua kwa ndege kubwa ya ya Emirate abiria
duniani ya A380 ya Ghorofa iliyotua katika uwanja wa Ndege wa Mwalumu
Julius Nyerere , jijini Dar es Salaam
Comments