Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger amepewa fursa kuwa mkufunzi tajiri zaidi duniani iwapo atajiunga na ligi kuu ya China.(Mirror)
Wenger ameombwa kuchukua wadhfa wa meneja mkuu katika klabu ya PSG(Le10 via Talksport)
Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho anasema kuwa kipa David de Gea hataondoka katika klabu hiyo mwisho wa msimu huu.
- Arsene Wenger: Nililazimishwa kuondoka Arsenal
- Atletico Madrid yalazimisha sare dhidi ya Arsenal uwanjani Emirates
- Real Madrid yailaza Bayern Munich Ujerumani
De Gea 27 anakamilisha mwaka wake wa mwisho wa kandarasi yake lakini United ina chaguo la kuongeza mwaka mwengine na wanajiandaa kwa mkataba mpya. (Manchester Evening News)
Mshambuiaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann, 27, anasema kuwa ameanza mazungumzo na klabu hiyo kuhusu hatma yake ya siku zijazo. Amehusishwa na Barcelona na Manchester United (Sun)
Mkufunzi wa Manchester City Pep Guardiola yuko tayari kumzuia Mikel Arteta kusalia miongoni mwa makocha wake licha ya raia huyo wa Uhispania kuhusishwa na Arsenal. (Mirror)
Mkufunzi wa Chelsea Antonio Conte huenda akakosa wadfha wa ukufuzi wa timu ya taifa ya Itali. Conte mwenye umri wa miaka 48 anataka mkataba mpya wa miaka mitano lakini shirikisho la soka nchini Itali limekataa kuafiia mahitaji hayo.(Times - subscription only)
Mkufunzi wa Newcastle Rafael Benitez anasema kuwa beki Jamaal Lascelles ni miongoni mwa wachezaji waliopo katika mipango yake ya siku za usoni. Mchezaji huyo amehusishwa na Chelsea pamoja na Liverpool. (Newcastle Chronicle)
Benitez amefungua mazungumzo ya kandarasi mpya na klabu hiyo kupitia washirikishi wake na anatumai kupata suluhu ya haraka ambayo itakuwa nzuri kwa kila mmoja.". (Times)
Mkufunzi wa Everton Sam Allardyce hajui iwapo beki wa Ufaransa Eliaquim Mangala ambaye ameichezea klabu hiyo mara mbili atapatiwa kandarasi ya kudumu baada ya kuwasili katika klabu hiyo kwa mkopo kutoka ManCity.(Liverpool Echo)
Mkufunzi wa Napoli Napoli Maurizio Sarri, ambaye amehusishwa na uhamisho wa Chelsea, ana kipengee katika kandarasi yake kinachomaanisha kwamba anaweza kuondoka kwa dau la £7m iwapo klabu hiyo ya Itali itapokea ombi kabla ya mwisho wa mwezi Mei.(London Evening Standard)
Tottenham ina mwezi mwengine kukamilisha mpangilio wa mechi za msimu ujao huku wakijiandaa kuanza kampeni mpya ya mechi za ugenini.. (London Evening Standard)
Comments