Mwenyekiti wa Bodi ya Mtandao wa Kijani Kibichi Tanzania (Mkikita), Dk. Kissui Steven Kissui (kulia) akimkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha kulelea Watoto Yatima cha HOCET, Hezekia Mwalugaja mfuko wa unga wa muhogo ikiwa ni sehemu ya tani 1.7 za unga huo unaozalishwa na Mkikita. Unga huo una thamani ya sh. mil. 3.3. Hafla hiyo imefanyika leo Makao Makuu ya Mkikita, Dar es Salaam.
Mwalugaja akiwashukuru Adama Ngamange na Dk. Kissui kwa msaada huo.
Meneja Uhusiano wa Mkikita, Neema Ngowi akielezea sababu zilizoifanya Mkikita kutoa msaada huo, ikiwemo kumshukuru Mungu kwa kuwawezesha kuanza kuzalisha unga huo.
Ngamange akiwa na baadhi ya Yatima wa Kituo cha Hocet ambao pia waliimba wimbo wa kuishukuru Mkikita kwa msaada huo.
Baadhi ya maofisa wa Mkikita
Hamida Shabaan wa Hocet akitoa shukrani kwa niaba ya yatima wenzie
Baadhi ya maofisa wa Mkikita wakiwa na jamii ya Hocet
Comments