Je wewe utafutilia
harusi ya kifalme ambayo itafanyika keshi Jumamosi kati mwanamfalme
Prince Harry na Meghan Markle au utatazama mechi ambayo ni fainali ya
mechi ya FA kati ya mahasimu Chelsea na Manchester United.
Mwanamfalme Prince William atakosa kuhudhuria fainali hiyo ya
kesho Jumamosi kwa kuwa ndiyo siku ya harusi ya nduguye Prince Harry. Prince William atakuwa msimamizi wa harusi ya nduguye huko Windsor kesho Jumamosi.
William amekuwa rais wa FA tangu mwaka 2006 na mara nyingi ndiye hupeana vikombe na medali.
Mjane wa Ray Wilkins Jackie atatoa kombe hilo kwa washindi huko Wembley.
- Prince Harry kumuoa mpenzi wake Meghan Markle
- Mgahawa Kenya watoza Sh1m kutazama harusi ya Prince Harry na Markle
Msemaji wa FA alisema: "Tunawatakia Prince William na wale watafunga ndoa siku njema."
Ray Wilkins ambaye alifariki mwezi uliopita akiwa miaka 61, alishinda kombe la FA kama mchezaji wa Manchester United mwaka 1983 na kufunga wakati wa fainali.
Pia alishinda kombe hilo mara tatu akiwa meneja wa Chelsea.
Comments