Wanafunzi wasulubiwa na kutandikwa viboko kwa kuchelewa Nigeria


Watu watatu wamekamatwa Nigeria kwa kutuhumiwa kuwafunga wanafunzi katika misalaba na kuwatandika viboko barabarani.
Watu hao watatu - akiwemo mwalimu mkuu - wanazuiwa baada ya polisi kupita na kushuhudia kisa hicho kuisni magharibi mwa jimbo la Ogun.
Picha zinaonyesha watu wawili - mmoja mvulana na miwngine msichana - waliofungwa kwenye msalaba kwa kamba ya kijani.
Msemaji wa polisi ametaja adhabu hiyo kama ya 'kiunyama'.
Taarifa katika eneo hilo zinasema walikuwa wanaadhibiwa kwa kuchelewa shuleni.
Afisa huyo - anayefahamika kwa jina moja tu Livinus - alijaribu kuingilia kati, akimtaka mwalimu mkuu awaachie wanafunzi hao .
Na wakati mwalimu mkuu huyo alipokataa afisa aliamua kuchukua hatua na aksukumwa nyuma kwa nguvu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

ALLY KAMWE AZIMIA KWA MKAPA.

RAIS SAMIA KUZINDUA MKUTANO MKUU WA 79 WA BARAZA LA MICHEZO YA MAJESHI DUNIANI

MIGINGO KISIWA KIDOGO ZAIDI AFRIKA KILICHOGOMBEWA NA UGANDA, KENYA