Watu watatu wamekamatwa Nigeria kwa kutuhumiwa kuwafunga wanafunzi katika misalaba na kuwatandika viboko barabarani.
Watu
hao watatu - akiwemo mwalimu mkuu - wanazuiwa baada ya polisi kupita na
kushuhudia kisa hicho kuisni magharibi mwa jimbo la Ogun.Picha zinaonyesha watu wawili - mmoja mvulana na miwngine msichana - waliofungwa kwenye msalaba kwa kamba ya kijani.
Msemaji wa polisi ametaja adhabu hiyo kama ya 'kiunyama'.
Taarifa katika eneo hilo zinasema walikuwa wanaadhibiwa kwa kuchelewa shuleni.
Afisa huyo - anayefahamika kwa jina moja tu Livinus - alijaribu kuingilia kati, akimtaka mwalimu mkuu awaachie wanafunzi hao .
Na wakati mwalimu mkuu huyo alipokataa afisa aliamua kuchukua hatua na aksukumwa nyuma kwa nguvu.
Comments