NMB YAGEUZA MAONESHO YA NANENANE KUWA DARASA

 Benki ya NMB imeendelea kuifanya Nanenane 2026 kuwa zaidi ya maonesho ya kilimo kwa kuendesha kampeni ya utoaji wa elimu ya kifedha, ujasiriamali na usimamizi wa biashara kwa wananchi waliotembelea mabanda yake katika kanda mbalimbali nchini.

Katika Banda la Vijana lililopo viwanja vya DK John Mwakangale jijini Dodoma, vijana wa mradi wa Building a Better Tomorrow (BBT) walipata mafunzo kuhusu namna ya kugeuza mawazo yao kuwa biashara endelevu, kusimamia fedha na kutumia huduma za kifedha kukuza shughuli za kilimo, ufugaji na uvuvi.

 Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mkuu wa Idara ya Kilimo kwa Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Christopher Mwalungenge, aliwahimiza vijana kuona kilimo kama biashara yenye fursa kubwa za kujenga kipato, ajira na ustawi wa muda mrefu.

Mbali na vijana, maafisa wa NMB waliendelea kutoa elimu kwa vikundi vya wakulima, wafugaji na wajasiriamali waliotembelea mabanda ya benki hiyo. Washiriki walipata uelewa kuhusu huduma za kifedha, mikopo ya sekta ya kilimo, bima pamoja na suluhisho zinazowawezesha kuongeza tija na kupanua biashara zao.

Kupitia elimu, ushauri na huduma za kifedha zinazotolewa katika mabanda yake, NMB imeendelea kuthibitisha nafasi yake kama mshirika wa maendeleo ya wakulima, wafugaji, wavuvi na vijana, huku ikichochea uchumi jumuishi unaojengwa kupitia maarifa na uwekezaji wenye tija. 





Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

Soma Taarifa ya UTEUZI:Rais Jakaya Kikwete amemteua Dkt. Ben E. Moshi kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya PUMA Energy (zamani ilijulikana kama BP Ltd)

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

MAAFISA JENERALI WASTAAFU 17 WA JWTZ WAAGWA.

BINTI WA KITANZANIA GLORIA MAJULE ASHINDA TUZO YA UANDISHI BORA WA FILAMU YA MALARIA MAREKANI ‎

HII NDIYO CV YA KOCHA MPYA WA YANGA

CDF MKUNDA AWATAKA MAAFISA JENERALI WASTAAFU KUACHA KUHANGAIKA NA SIASA

KOCHA WA MC ALGERS AIHOFIA YANGA

MAMBO 16 USIYOYAJUA KUHUSU RAIS MSTAAFU DKT. JAKAYA KIKWETE

HIZI HAPA TAKWIMU ZA PETER SHALULILE MCHEZAJI MPYA WA YANGA SC 🔰 🔥