REKODI YA SIMBA NA YANGA TANGU MWAKA 2010



P W D L GF GA GD Pts
Yanga SC 12 4 5 3 14 15 -1 12
Simba SC 12 3 5 4 15 14 1 9
Kiungo wa Simba SC, Mwinyi Kazimoto akimtoka kiungo wa Yanga SC, Thabani Kamusoko timu hizo zilipokutana mara ya mwisho

APRILI 18, 2010
Simba Vs Yanga
4-3
WAFUNGAJI:
SIMBA: Uhuru Suleiman dk 3, Mussa Mgosi dk 53 na 74, Hillary Echesa dk 90+  
YANGA: Athumani Iddi dk 30, Jerry Tegete dk 69 na 89 
OKTOBA 16, 2010:
Yanga Vs Simba
1-0
MFUNGAJI: Jerry Tegete dk 70
MACHI 5, 2011
Simba Vs Yanga
1-1
WAFUNGAJI:
YANGA: Stefano Mwasyika (penalti) dk 59. 
SIMBA:  Mussa Mgosi dk 73.
(Refa Orden Mbaga alizua tafrani uwanjani, kwanza kwa kulikataa bao la kusawazisha la Simba, kisha akalikubali baada ya kujadiliana na msaidia wake namba moja)
OKTOBA 29, 2011
Yanga 1-0 Simba
MFUNGAJI: Davies Mwape dakika ya 75
MEI 6, 2012
Simba 5-0 Yanga SC
WAFUNGAJI: 
Emmanuel Okwi (dk 2 na 62), Felix Sunzu (penalti 56), Juma Kaseja (penalti dk 67) na Patrick Mafisango (penalti dk 72)
(Ligi Kuu)
OKTOBA 3, 2013
Simba 1-1 Yanga SC
WAFUNGAJI:
Simba SC: Amri Kiemba dk3
Yanga SC: Said Bahanuzi dk65
(Ligi Kuu)
MEI 18, 2013
Yanga 2-0 Simba SC
WAFUNGAJI: Didier Kavumbangu dk 5 na Hamisi Kiiza dk 62.
OKTOBA 20, 2013
Yanga SC 3-3 Simba SC
WAFUNGAJI:
Yanga SC: Mrisho Ngassa dk15, Hamisi Kiiza dk36 na 45
Simba SC: Betram Mombeki dk54, Joseph Owino dk58 na Gilbert Kaze dk85.
APRILI 19, 2014
Simba SC 1-1 Yanga SC
WAFUNGAJI:
Simba SC; Haroun Chanongo dk76
Yanga SC: Simon Msuva dk86
OKTOBA 18, 2014
Simba SC 0-0 Yanga SC
MACHI 8, 2015
Simba 1-0 Yanga SC
MFUNGAJI; Emmanuel Okwi dk52
SEPTEMBA 26, 2015
Yanga SC 2-0 Simba SC
WAFUNGAJI: Amissi Tambwe dk44 na Malimi Busungu dk79
Mashabiki wa Yanga SC wakifurahia ushindi wa 2-0 Septemba 26, mwaka jana. Je, furaha itaendelea na kesho?

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
JUMLA ya mechi 12 za watani wa jadi, Simba za Yanga SC za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara zimechezwa tangu mwaka 2010.
Yanga SC wameshinda mechi nne, Simba SC wameshinda mechi tatu, wakati mechi tano zilimalizika kwa sare.
Kitu kimoja tu Simba SC wanajivunia kwa muongo huu hadi sasa ni kuvuna mabao 15 ndani ya mechi hizo mahasimu wao waliofunga mabao 14 licha ya kuongoza kushinda idadi ya mechi.
Ushindi wa mabao 5-0 waliopata Simba SC dhidi ya mahasimu wao hao, Mei 6, mwaka 2012 unabaki kuwa ushindi mkubwa zaidi baina ya miamba hiyo kwa muongo huu hadi sasa.
Siku hiyo, mabao ya Simba SC yalifungwa na Emmanuel Okwi dakika ya pili na 62, Felix Sunzu kwa penalti dakika ya 56, Juma Kaseja kwa penalti dakika ya 67 na Patrick Muteesa Mafisango (sasa marehemu) kwa penalti pia dakika ya 72.
Kipigo hicho kililipa deni la Simba SC la Juni 1, mwaka 1968 walipofungwa 5-0 pia na mahasimu wao hado, mabao ya Maulid Dilunga (sasa marehemu) dakika ya 18 kwa penalti na 43, Salehe Zimbwe dakika ya 54 na 89 na Kitwana Manara dakika ya 86.
Lakini bado kipigo kikali zaidi kihistoria kwa mechi za watani wa jadi kinabaki kuwa cha Julai 19, mwaka 1977, Simba ilipoitandika Yanga SC
6-0, Alhaj Abdallah Athumani Seif ‘King Kibadeni’ akifunga mabao matatu peke yake dakika za 10, 42 na 89, Jumanne Hassan 'Masimenti' mawili dakika ya 60 na 73 na Suleiman Sanga aliyejifunga dk. 20.
Donald Ngoma amelala chini, Hassan Kessy anaondoka na mpira Septemba 26, mwaka jana

Mechi ya kwanza ya mahasimu muongo huu, ilichezwa Aprili 18, mwaka 2010 na Simba ikashinda 4-3, mabao yake yakifungwa na Uhuru Suleiman dakika ya tatu, Mussa Hassan Mgosi dakika ya 53 na 74 na Hillary Echesa dakika ya 90 na ushei, wakati ya watani wao yalifungwa na Athumani Iddi ‘Chuji’ dakika ya 30 na Jerry Tegete dakika ya 69 na 89. 
Mechi iliyofuata Oktoba 16, 2010, bao pekee la Jerson John Tegete dakika ya 70 lilitosha kuipa Yanga SC ushindi wa 1-0 Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza. Mchezo uliofuata timu hizo zilitoka sare ya 1-1 Machi 5 mwaka 2011, Yanga SC wakitangulia kupata bao kwa penalti lililofungwa na Stefano Mwasyika dakika ya 59, baada ya Juma Nyosso kumuangusha Davies Mwape, kabla ya Mussa Mgosi kuisawazishia Simba SC dakika ya73.
Siku hiyo, refa Orden Mbaga alizua tafrani Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kutokana na kwanza kwa kulikataa bao la kusawazisha la Simba, kisha akalikubali baada ya kujadiliana na msaidizi wake namba moja.
Mchezo uliofuata Mzambia, Davies Mwape akafunga bao pekee dakika ya 75 Oktoba 29 mwaka 2011, Yanga SC ikishinda 1-0, kabla ya Simba SC kuwashughulikia ‘kiroho mbaya’ watani wao hao katika mchezo uliofuata Mei 6 mwaka 2012 kwa kuwatandika 5-0.
Oktoba 3, mwaka 2013 timu hizo zilitoka sare ya 1-1, bao la Simba SC likifungwa na Amri Kiemba dakika ya tatu, kabla ya Yanag SC kusawazisha kupitia kwa Said Bahanuzi kwa penalti dakika ya 65.
Amissi Tambwe anaambaa na mpira Septemba 26 Uwanja wa Taifa

Ukawadia mchezo ambao ulimfukuzisha kipa Juma Kaseja Simba SC baada ya Wekundu wa msimbazi kuchapwa 2-0 Mei 18, mwaka 2013, mabao ya Mrundi Didier Kavumbangu dakika ya tano na Mganda Hamisi Kiiza dakika ya 62.
Oktoba 20, mwaka 2013 Yanga SC iliongoza kwa mabao 3-0 hadi mapumziko yaliyofungwa na Mrisho Khalfan Ngassa dakika ya15 na Hamisi Kiiza dakika ya 36 na 45, kabla ya Simba SC kusawazisha yote kipindi cha pili kupitia kwa Betram Mombeki dakika ya 54, Mganda Joseph Owino dakika ya 58 na Mrundi Gilbert Kaze dakika ya 85.
Aprili 19, mwaka 2014 timu hizo zilitoka tena sare ya 1-1, Haroun Chanongo akitangulia kuifungia Simba SC dakika ya kabla ya Simon Msuva kuisawazishia Yanga SC dakika ya 86, wakati Oktoba 18 mwaka 2014 zilitoka 0-0.
Bao la Mganda Emmanuel Arnold Okwi dakika ya 52, lilitosha kuipa Simba SC ushindi wa 1-0 Machi 8, mwaka 2015 – wakati mchezo wa mwisho kuzikutanisha timu hizo, Yanga SC ilishinda 2-0 Septemba 26, mwaka 2015 mabao ya Amissi Tambwe dakika ya 44 na Malimi Busungu dakika ya 79.
Hiyo ilikuwa mechi ya 12 ya watani wa jadi kufanyika tangu mwaka 2010 katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Yanga SC wakishinda kwa mara ya nne dhidi ya mara tatu za Simba SC. Timu hizo zinatarajiwa kukutana tena Jumamosi katika mfululizo wa Ligi Kuu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Hivi unaposoma makala haya, Simba SC wapo kambini mjini Morogoro, wakati Yanga SC wapo kisiwani Pemba kwa maandalizi ya mchezo huo. Miaka miwili ya nyuma, Simba SC dhaifu ndiyo imekuwa ikikutana na Yanga SC pamoja na matokeo yote – lakini kuelekea mchezo wa Jumamnosi hali ni tofauti.
Malimi Busungu alitokea benchi na kutoa pasi ya bao la kwanza lililofungwa na Tambwe, kabla ya yeye mwenyewe kufunga la pili Septemba 26

Simba SC sasa imeimarika chini ya kocha Mganda, Jackson Mayanja ikiwa inaongoza Ligi Kuu kwa pointi zake 45 dhidi ya 43 za mahasimu, Yanga SC. Na wakizingatia wamecheza mechi moja zaidi ya Yanga, Simba SC wanajua ili kuimarisha mawindo yao ya ubingwa ambao mara ya mwisho waliutwaa mwaka 2011 ni kiasi gani wanahitaji kushinda Jumamosi.    
Na Yanga SC wanataka kushinda ili kurudi kileleni na kuweka hai matumaini ya kutetea ubingwa wao na hapo ndipo unapogundua kwamba mchezo wa Jumamosi ni mtamu zaidi kuwahi kutokea kwa muongo huu. 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA