SPIKA TULIA AITAKA JAMII KUONDOKANA NA DHANA KWAMBA MWANAMKE NI MNYONGE


 Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, ameitaka Jamii kuondokana na dhana ya kwamba Mwanamke ni mnyonge anayetakiwa kusaidiwa bali apewe nafasi kutokana na Uwezo wake.


Aidha, amesisitiza Viongozi Wanawake kuondokana na mtazamo wa kwamba wao pia ni wahanga wa ubaguzi wa kijinsia bali waongeze ujasiri na jitihada za kukabiliana na changamoto wanazopitia, ili kuwahamasisha mabinti na watoto wakike kujitambua kuwa wao pia wanaweza.


Dkt. Tulia ameyasema hayo wakati akishiriki katika Mkutano wa Jukwaa la Kibunge la Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC-PF) unaoendelea leo tarehe 3 Julai, 2024 Luanda nchini Angola.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

RAS KILIMANJARO NA DEREVA WAFARIKI KWA AJALI, MKUU WA MKOA ADHIBITISHA

WACHEZAJI WAGENI WA YANGA HAWA HAPA...

BALOZI NCHIMBI MSIBANI KWA TIXON NZUNDA

SERIKALI YAIPA TANROADS BIL 58.27 KUJENGA DARAJA LA SIMIYU NA SUKUMA

JKCI YASHIRIKI KAMPENI YA AFYA CHECK KUTOA HUDUMA ZA MATIBABU YA MOYO

BALOZI NCHIMBI AONGOZA MAPOKEZI YA KATIBU MKUU, MGOMBEA URAIS WA FRELIMO

BALOZI NCHIMBI AWAONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA NZUNDA SONGWE

CRDB BUNGE BONANZA LAFANA DODOMA