RIPOTI YA UJENZI WA SEKONDARI MPYA MUSOMA VIJIJINI*


1. Idadi ya Sekondari Jimboni mwetu:

        (Kata 21 zenye Vijiji 68)


1a. Sekondari za Kata/Serikali: 26

1b. Sekondari za Madhehebu ya Dini: 2

1c. "High Schools": 1

1d. "High Schools" mpya za sayansi: 2


*Malengo ya Musoma Vijijini:*

*Kila kijiji kiwe na Shule za Msingi za kutosha

*Kila kijiji kiwe na Sekondari moja


2. Sekondari mpya zitakazofunguliwa 2025


2a. Zinazojengwa na Serikali: 3

       (Vijijini: Butata, Kasoma & Kurwaki)

2b. Zinazojengwa na wanavijiji: 3

        (Vijijini: Muhoji, Nyasaungu &

                                           Kisiwani Rukuba)


3. Sekondari mpya zilizoanzwa kujengwa mwaka huu (2025) kwa nguvu za wanavijiji: 6


3a. Chitare Sekondari, Kata ya Makojo

3b. Mmahare Sekondari, Kata ya Etaro

3c. Kataryo Sekondari, Kata ya Tegeruka

3d. Nyabakangara, Kata ya Nyambono

3e. Mwigombe Tech, Kata ya Kiriba

3f: Musanja Sekondari, Kata ya Musanja


Fedha za Mfuko wa Jimbo:

Kila moja ya hizo sekondari sita (6) tayari imepewa Saruji Mifuko 150, na nyingine zimepewa nondo


4. HARAMBEE ZA MBUNGE:


Mbunge wa Jimbo ameishapiga Harambee za kutafuta vifaa vya ujenzi wa sekondari zifuatazo:


4a: Chitare: mifuko ya saruji

       Wanakijiji 50, Mbunge 150


4b. Mmahare: mifuko ya saruji

       Wanakijiji 155, Mbunge 155


4c. Mwigombe Tech: mifuko ya saruji

       Wanakijiji 182, Mbunge 200

       Familia Mashenene: inajenga darasa


Mbunge wa Jimbo ameanza kutoa mifuko ya saruji (ahadi zake binafsi) kwa vijiji vilivyoanza ujenzi unaonekana na kufuatiliwa ipasavyo.


   4d. Tarehe za Harambee zijazo:


*Nyabakangara Sekondari, Kijijini Nyambono

Tarehe 25 Machi 2025

Saa 8 mchana


*Kataryo Sekondari, Kijijini Kataryo 

Tarehe 26 Machi 2025

Saa 8 mchana


*Musanja Sekondari, Kijijini Musanja

Tarehe 27 Machi 2025

Saa 8 mchana 


VIDEO/CLIP iliyoambatanishwa hapa inaonesha:

Wanakijiji wakiwa kazini Kijijini Chitare, Kata ya Makojo. Matofali 3,750 tayari yamefyatuliwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Chitare Sekondari. Hii ni sekondari ya pili ya Kata hii ya Makojo.


Ofisi ya Mbunge 

Jimbo la Musoma Vijijini 

www.musomavijijini.or.tz 


P. O. Box 6

Musoma 


Tarehe:

Jumamosi, 15 Machi 2025

13:00 hrs

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

RAIS TRUMP ARARUANA NA RAIS WA UKRAINE

MWABUKUSI ATOA NENO SIMBA KUSUSIA DERBY DHIDI YA YANGA

SERIKALI YALIKUBALI OMBI LA DIAMOND

HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO

ARAJIGA AULA KOMBE LA DUNIA