GEITA YATAMBA KUWA NDANI YA KUMI BORA KWA MAFANIKIO

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari MAELEZO, Rodney Thadeus akitoa neno la kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kihongosi kuzungumza na waandishi wa habari.

Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo.


MUHTASARI WA MAFANIKIO YA MKOA WA GEITA

WASIFU WA MKOA

 

Utangulizi

Mkoa wa Geita una eneo la kilometa za mraba 21,879 (Geita 6,375 km2, Bukombe 6,798 km2, Chato 3,572 km2, Mbogwe 3,684 km2, na Nyang`hwale 1,450 km2), kati ya hizo kilomita za mraba 19,933 ni za nchi kavu na kilomita za mraba 1,946 ni za maji. Mkoa una Wilaya tano (5), Majimbo tisa (9) ya uchaguzi, Halmashauri sita (6), Miji midogo 2, Tarafa 20, Kata 122, Vijiji 486, Vitongoji 2,195 na Mitaa 65. Wilaya hizo ni Geita, Nyang’hwale, Chato, Bukombe na Mbogwe. Mkoa unajumuisha Halmashauri ya Manispaa ya  Geita, Halmashauri za Wilaya za Geita, Nyang’hwale, Chato, Bukombe na Mbogwe. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Mkoa wa Geita una wakazi wapatao 2,977,608 ambapo Wanaume ni 1,463,764 na Wanawake ni 1,513,844.

 

Hali ya Uchumi.

Hali ya Uchumi ya Mkoa imeendelea kuimarika ambapo Pato halisi lilikua kutoka Shilingi 7,031,590,000/= mwaka 2021 hadi Shilingi 9,122,637,000/= mwaka 2024 sawa na ukuaji wa asilimia 31 Vilevile, pato la mtu mmoja mmoja limeongezeka kutoka shilingi 2,769,308/= mwaka 2021 hadi shilingi 2,814,714/= mwaka 2024 sawa na ongezeko la asilimia 1.6.

Ulinzi na Usalama

Hali ya ulinzi na usalama  katika Mkoa imeendelea kuwa  shwari  kutokana na ushirikiano uliopo baina ya vyombo vya Dola na Wananchi. Hali hii imewawezesha wananchi kuishi kwa amani na utulivu na kuendelea na shughuli zao za kiuchumi, kijamii na kisiasa.

MAFANIKIO YA SERIKALI YA AWAMU YA SITA KATIKA MKOA WA GEITA

Mkoa wa Geita umepata mafanikio makubwa katika nyanja na sekta zote. Mafanikio hayo yametokana na uimara wa Chama cha CCM katika kuendelea kuisimamia Serikali kwa lengo la kuhakikisha inatekeleza na kutoa fedha kwa ajili ya shughuli za maendeleo.  Kutokana na hilo, kwa kipindi cha kuanzia machi 2021 – Juni, 2025, Mkoa umepokea Shilingi trilioni  1,442,899,340,734/= kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo katika sekta za afya, elimu, miundombinu ya usafiri na usafirishaji, maji, nishati, kilimo, mifugo, uvuvi, misitu, utalii, viwanda, biashara, uwezeshaji wananchi kiuchumi na miradi ya kimkakati. Baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika kipindi husika ni kama ifuatavyo:

 

Huduma za Jamii

Afya

Mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na kuimarika kwa miundombinu ya kutolea huduma za afya, kuongezeka kwa upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi na kuimarika kwa upatikanaji wa huduma za afya karibu na wananchi. Mafanikio hayo ni pamoja na:

(a)        Kukamilika kwa ujenzi wa Hospitali za Halmashauri za Bukombe, Chato, Geita, Geita Manispaa, Mbogwe na Nyang’hwale;(a)        Kukamilika kwa ujenzi wa majengo matatu (3) ya huduma za dharura (EMD) katika Hospitali ya Bukombe, Katoro na Hospitali ya Halmashauri Nyang’hwale;

(b)        Kukamilika kwa ujenzi wa jengo la wagonjwa mahututi katika Hospitali ya Halmashauri ya Geita (Nzera) na ukarabati wa Hospitari ya Halmashauri ya Bukombe na  Manispaa ya Geita;

(c)        Kuongezeka kwa idadi ya zahanati kutoka 129 mwaka 2021 hadi 198 mwaka 2025;

(d)        Kuongezeka kwa vituo vya afya kutoka 25 mwaka 2021 hadi 42 mwaka 2025;

(e)        Kuongezeka kwa nyumba za watumishi wa afya kutoka 180 mwaka 2021 hadi 230 mwaka 2025;

(f)         Kuongezeka kwa upatikanaji wa dawa, vifaa, vifaa tiba na vitendanishi katika vituo vya kutolea huduma za afya kutoka asilimia 80 mwaka 2021 hadi asilimia 90 mwaka 2025;

(g)        Kupunguza vifo vya mama wajawazito kutoka 57 mwaka 2021 hadi vifo 55 mwaka 2025; na

(h)        Kupunguza maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kutoka 5.1% mwaka 2021 hadi kufikia 4.90% mwaka 2025.

Elimu

Mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya elimu yamewezesha kuongezeka kwa uandikishaji na udahili wa wanafunzi, ufaulu pamoja na kupunguza umbali wa wanafunzi kufuata huduma ya elimu. Mafanikio hayo ni pamoja na:

(a)  Kuendelea kutekeleza Mpango wa Elimu bila Ada kuanzia elimu ya awali hadi kidato cha sita kwa kuongeza fedha za kugharamia mpango huo kutoka Shilingi 6,486,387,724.00/= mwaka 2021 hadi Shilingi 19,989,544,192/=mwaka 2025;

(b)  Kuongezeka kwa idadi ya shule za msingi na Awali kutoka 641 mwaka 2021 hadi 792 mwaka 2025;

(c)  Kuongezeka kwa idadi ya shule za sekondari kutoka 130 mwaka 2021 hadi 240 mwaka 2025;

(d)  Kuongezeka kwa idadi ya vyumba vya madarasa ya shule za msingi na sekondari kutoka madarasa 7,206 mwaka 2021 hadi 10,540 mwaka 2025;

(e)  Kuongezeka kwa nyumba za walimu wa shule za msingi na sekondari kutoka 2,272 mwaka 2021 hadi 2,375 mwaka 2025;

Kuongezeka kwa uandikishaji wa wanafunzi wa elimu ya awali kutoka wanafunzi 73,446 mwaka 2021 hadi wanafunzi 227,087 mwaka 2025, darasa la kwanza kutoka 107,519 mwaka 2021 hadi 334,224 mwaka 2025, kidato cha kwanza kutoka 37,834 mwaka 2021. (a)  hadi 131,645 mwaka 2025, kidato cha tano kutoka 1,900 mwaka 2021 hadi 2,618 mwaka 2025;

(b)        Kuimarika kwa ufaulu kwa wanafunzi wa darasa la saba kwa asilimia 82.49 mwaka 2021 na asilimia 71.53 mwaka 2024, kidato cha nne asilimia 84.56 mwaka 2021 na asilimia 94.45 mwaka 2024 na kidato cha sita kwa asilimia 99.98 mwaka 2021 na asilimia 99.96 mwaka 2024;

(c)         Idadi ya walimu katika ngazi ya elimu ya msingi imeongezeka kutoka 8,876 mwaka 2021 hadi 9,156 mwaka 2025 na elimu sekondari kutoka walimu 3,398 mwaka 2021 hadi 3,696 mwaka 2025;

(d)        Kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu ya vyuo vya kati (VETA) kutoka chuo kimoja mwaka 2021 hadi vyuo 05 mwaka 2025, vyumba vya maabara kutoka 165 mwaka 2021 hadi 338 mwaka 2025. Aidha, mabweni ya wasichana 74 katika shule za sekondari, mabwalo 19 na hosteli 5; majengo ya utawala 12, matundu ya vyoo 14,133, yamejengwa na kukamilika;

(e)        Kuongezeka kwa Wanafunzi wa MEMKWA walioandikishwa kutoka 2,169 mwaka 2021 hadi wanafunzi 2,269 mwaka 2025; na

(f)         Kuongezeka kwa Wanafunzi wenye mahitaji Maalum kwa shule za msingi na sekondari kutoka wanafunzi 1,052 mwaka 2021 hadi wanafunzi 2,233 mwaka 2025.

Maji

Katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 hadi 2025 Serikali ya awamu ya sita iliweka kipaumbele cha kuendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kaya nyingi zaidi zinaunganishwa na huduma ya maji. Katika kutekeleza azma hiyo mafanikio makubwa yamepatikana Mkoani Geita kama ifuatavyo:

(a)        Kuimarika kwa huduma ya upatikanaji wa maji safi kwa wananchi wa Mkoa kutoka 65% mjini na 61% vijijini mwaka 2021 hadi asilimia 75% mjini na 65% vijijini mwaka 2025;

(b)        Kuongezeka kwa uzalishaji wa maji katika Mji wa Geita kutoka lita milioni 5,200,000 kwa siku mwaka 2021 hadi 6,800,000 kwa siku mwaka 2025;

(c)         Kuongezeka kwa idadi ya vijiji vyenye huduma ya maji kutoka Vijiji 204    mwaka 2021 hadi Vijiji 420 mwaka 2025;

(d)        Kukamilika kwa miradi 81 na kuanza kutoa huduma ya maji kwa wananchi waishio vijijini na kuendelea na utekelezaji wa miradi 20 iliyofikia wastani wa asilimia 51 chini ya usimamizi wa RUWASA; na kukamilika kwa miradi 3 ya maji na kuendelea kutekeleza miradi 4 iliyofikia wastani wa asilimia 60 chini ya usimamizi wa GEUWASA; na

(e)        Kuongezeka kwa kasi ya uchimbaji wa visima vya maji kutoka visima 299  mwaka 2021 hadi visima 389 mwaka 2025;

 

              Aidha chini ya usimamizi wa GEUWASA imetekelezwa miradi ifuatayo:- a)    Ujenzi wa mradi wa maji Bulera - Nyaseke utakaohudumia wakazi 5,000 katika vijiji vya Bulera, Nyaseke na Gamashi;

b)    Ujenzi wa mradi wa maji Bung'wangoko utakaohudumia wakazi 6,200 katika vijiji vya Chabulongo, Bung'wangoko center na Mshinde;

c)    Utanuzi wa Chujio la maji (Treatment Plant) Nyankanga;

d)    Ujenzi wa mradi wa maji Mbogwe - Msumbwe utakaohudumia wakazi 7,200 katika maeneo ya Kagri, Masumbwe na Nyakafuru;

e)    Utanuzi wa mtandao wa maji kata ya Mbogwe na Iponya utakaohudumia vijiji vya Bwendanseko, Nyambubi, Buluhe na Nyashimba;

f)     Ujenzi wa mradi wa maji katoro - Buseresere ambao umekamilika na unahudumia wakazi wa Katoro, Ludete Nyamigota na Buseresere. Mradi umesanifiwa kuhudumumia wakazi 68,000; na

g)    Ujenzi wa mradi wa maji kutoka Ziwa Viktoria - Miji 28 utakahudumia kata 13 za Mji wa Geita na vijiji 19 vya Geita DC ambayo vinapitiwa na mradi. Aidha utekekelezaji wake unandelea.

Sekta za Uzalishaji

Kilimo

Serikali ya awamu ya sita  imeendelea kutekeleza shughuli za kilimo katika Mkoa wa Geita kwa kuhakikisha kilimo kinakuwa chenye tija na usalama wa chakula unaimarika. Katika kusimamia hilo mafanikio mbalimbali yamepatikana ikiwemo:

(a)        Kuanzishwa  kwa skimu za umwagiliaji na kufikia skimu 02 mwaka 2025;

(b)        Kuimarika kwa hali ya upatikanaji wa mbolea ya ruzuku kutoka tani 1,684.67 mwaka 2021 hadi tani 5,934.05 mwaka 2025;

(c)        Kuimarisha huduma za ugani kwa kununua vitendea kazi ikiwemo pikipiki 153 vipima udongo 5 na vishikwambi 175 kwa ajili ya maafisa ugani;

(d)        Kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya chakula kutoka tani 1,445,814 mwaka 2021 hadi tani 1,512,761mwaka 2025 na mazao ya biashara kutoka tani 67736 mwaka 2021 hadi tani 72820 mwaka 2025;

(e)        Kuimarisha ushiriki wa vijana katika kilimo kwa kutoa mafunzo na ujenzi wa vitalu nyumba kwa vijana 600 mwaka 2021 na Vijana 662 kwa mwaka 2025;

(f)         Kuongezeka kwa vyama vya ushirika kutoka 512 na wanachama 44,375 mwaka 2021 hadi vyama vya ushirika 600 na wanachama 49,875 mwaka 2025;

(g)        Kuongeza uzalishaji wa zao la pamba kutoka tani 9,309 mwaka 2021 hadi tani 19,632 mwaka 2025; na (a)        Kuongeza uzalishaji wa zao la mahindi kutoka tani 326,088 mwaka 2021 hadi tani 372,199 mwaka 2025;

 

Mifugo

Serikali ya awamu ya sita chini ya usimamizi wa Chama Cha Mapinduzi inatambua umuhimu wa sekta ndogo ya Mifugo kama shughuli kuu ya kiuchumi kwa wakazi wa Mkoa. Kutokana na umuhimu huo, Serikali ya Mkoa wa Geita katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 had 2025 imeendelea kuhimiza ufugaji wa kisasa wenye kuzingatia kinga, tiba na utafiti wa mifugo ili ufugaji uweze kuwanufaisha wananchi. Mafanikio yaliyopatikana ni ka ifuatavyo:-

(a)        Kusambaza dawa za ruzuku za kuogeshea mifugo lita 839 na dozi 770,000 za chanjo ya kudhibiti ugonjwa wa homa ya mapafu ya ng’ombe (CBPP);

(b)        Kukamilika kwa ujenzi wa jumla ya majosho 13 katika Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Geita, Geita Manispaa, Mbogwe na Nyang’hwale kwa ajili ya kuogesha mifugo;

(c)        Kuimarisha huduma za ugani kwa kugawa pikipiki 43 kwa maafisa mifugo;

(d)        Kuanzisha mashamba darasa ya malisho ya mifugo yapatayo hekta 64 sawa na ekari 160;

(e)        Kutoa elimu ya ufugaji bora na uboreshaji wa mbari za mifugo kwa kusambaza mbegu bora za mifugo zipatazo 2,000 kwa njia ya uhimilishaji;(a)        Kuongezeka kwa uzalishaji wa maziwa kutoka lita 31,952,400 mwaka 2021 hadi 35,836,800 mwaka 2025; na

(b)        Kuongezeka kwa uzalishaji wa nyama kutoka tani 4,626,375 mwaka 2021 hadi tani 7,710,625 Mwaka 2025;

 

Uvuvi

Kwa kipindi cha mwaka 2021 hadi 2025 Mkoa umetekeleza majukumu yake kwa mujibu wa Ilani ya chama cha mapinduzi ya mwaka 2020-2025 sura ya pili ibara ya 43 kifungu kidogo cha (h na o). Mkoa umeimarisha vikundi vya vyama vya ushirika na kwa lengo la kupata mitaji na hivyo kuongeza tija katika shughuli za uvuvi.

a)    Idadi ya wavuvi imeongezeka kutoka 7,549 mwaka 2021 hadi 10,001 mwaka 2025; na

b)    Idadi ya vyombo vya uvuvi imeongezeka kutoka 997 mwaka 2021 hadi 2,500 mwaka 2025

Shughuli za Ufugaji samaki

Mkoa umeimarisha vikundi vya ufugaji samaki na kituo cha kuendeleza ukuzaji viumbe maji cha Lubambangwe kwa lengo la kukuza sekta ya ufugaji samaki.

a)    Idadi ya vizimba vya kufugia Samaki imeongezeka kutoka 4 mwaka 2021 hadi vizimba 27 mwaka 2025; naa)    Mitaji iliyotolewa na Serikali kwa wafugaji wa Samaki imeongezeka kutoka shilingi 14,000,000 mwaka 2021 hadi shilingi 792,563,616.24 mwaka 2025.

 

Madini

Serikali ya awamu ya sita inatambua kuwa sekta ya madini ina nafasi ya kipekee katika kuchangia ukuaji wa Pato la Taifa, upatikanaji wa fedha za kigeni na ukuaji wa uchumi kwa ujumla. Kwa Mkoa wa Geita, Mafanikio yaliyopatikana kutokana na sekta ya madini ni kama ifuatavyo:-

(a)        Kuongezeka kwa uzalishaji wa madini kutoka tani 18.21 mwaka 2021 hadi tani 27.43  mwaka 2025;

(b)        Kuongezeka kwa fedha za kigeni zilizotokana na uuzaji wa madini kutoka Dola za Marekani 72,878,325.91 mwaka 2021 hadi Dola za Marekani 92,204,527.35 mwaka 2025;

(c)        Kuongezeka kwa mapato ya Halmashauri yatokanayo na uchimbaji wa madini kutoka Shilingi  6,163,170,093.30 mwaka 2021 hadi Shilingi  10,582,192,189.88 mwaka 2025;

(d)        Kuongezeka kwa masoko ya madini kutoka masoko 10 mwaka 2021 hadi masoko 20 mwaka 2025; na

(e)        Kuongezeka kwa utoaji wa leseni kwa wachimbaji wadogo kutoka leseni 903  mwaka 2021 hadi  9,774 mwaka 2025.

Viwanda na Biashara

Kwa kipindi cha uongozi wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mafanikio yaliyopatikana katika skta hii ni pamoja na:

(a)        Kuongezeka kwa viwanda kutoka 824 mwaka 2021 hadi viwanda 1,542 mwaka 2025;

(b)        Kuongezeka kwa ajira za viwandani, kutoka ajira 927 mwaka 2021 hadi ajira 15,161 mwaka 2025; na

(c)        Kuongezeka kwa utoaji wa leseni kwa wafanya biashara kutoka leseni 1,346 mwaka 2021 hadi leseni 2,815 mwaka 2025.

 

Sekta ya Miundombinu

Katika kipindi cha kuanzia mwaka 2021 hadi 2025 Serikali imendelea na ujenzi wa miundombinu mbalimbali ikiwemo barabara, madaraja na makalvati ili kuimarisha shughuli za kiuchumi na kijamii.  Mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na:

(a)  Kuongezeka kwa mtandao wa barabara za lami kutoka kilomita 450.86 mwaka 2021 hadi kilomita 476.87 mwaka 2025;

(b)  Kuongezeka kwa mtandao wa barabara za changarawe kutoka kilomita 1,984.18 mwaka 2021 hadi 3,078.48 mwaka 2025;(a)  Kukamilika kwa ujenzi wa madaraja 28 katika Wilaya za Geita, Bukombe, Chato, Mbogwe na Nyang’hwale;

(b)  Kukamilisha ujenzi wa makalavati 3,444 katika Wilaya za Geita, Bukombe, Chato, Mbogwe na Nyang’hwale;

(c)  Kusimika taa za barabarani kutoka taa 589 mwaka 2021 hadi taa 323 mwaka 2025;

(d)  Kukamilika kwa ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Geita kilichopo Wilaya ya Chato;

(e)  Kukamilisha ujenzi wa madaraja 6 katika Wilaya za Geita na  Chato;

(f)   Kuendelea na utekelezaji wa mradi wa TACTIC katika Manispaa ya Geita unaohusu uboreshaji wa barabara ya urefu wa km 17 kwa kiwango cha lami;

Sekta ya Nishati

Sekta ya nishati imeendelea kuwa mhimili muhimu katika kuwezesha utekelezaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Geita. Kutokana na hilo, CCM iliisimamia Serikali katika kuhakikisha kuwa Mkoa unakuwa na nishati ya kutosha ili kukidhi mahitaji ya kiuchumi na kijamii. Mafanikio yaliyopatikan ni pamoja na:

(a)        Kuunganisha umeme kutoka vijiji 386 mwaka 2021 hadi vijiji 483 mwaka 2025. Aidha, mradi huu wa umeme umeweza kuunganisha umeme katika vitongoji 1,021 kati ya vitongoji 2,195 sawa na asilimia 46.5;(a)        Kukamilika kwa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Geita hadi Nyakanazi ambayo iliendana na kuunganisha umeme katika vijiji 4  na vitongoji 29 vilivyoko pembezoni mwa njia hiyo katika mkoa wa Geita;

(b)        Kuendelea na utekelezaji wa mkakati wa nishati safi ya kupikia ambao umelenga kuboresha afya ya jamii na kulinda mazingira safi ya kupikia kwa kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia na kugawa mitungi 16,275  ya gesi kwa mamalishe/wananchi;

(c)        Kukamilika kwa mradi wa kusambaza umeme vijijini (REA3R2) ambao ulipeleka umeme katika vijiji 127 `na vitongoji 50;

(d)        Kukamilika kwa mradi wa kusambaza umeme maeneo yaliyo pembezoni mwa miji (Peri urban ) ambao ulifanikiwa kusambaza umeme katika  mitaa na vitongoji  45 vilivyo pembezoni mwa Manispaa ya Geita;

(e)        Kufanikisha  maboresho ya miundombinu ya usambazaji umeme katika wilaya zote za mkoa wa Geita kwa kuondoa nguzo za miti na kuweka za zege ambazo zinadumu kwa  muda mrefu zaidi;

(f)         Kujenga njia za kusambaza umeme katika maeneo 52 ya wachimbaji madini wadogo wa Mkoa wa Geita na hivyo kuwapunguzia gharama za uendeshaji katika machimbo yao kwani awali walitumia gharama kubwa katika kununua mafuta;

Sekta ya Maliasili na Utalii

Serikali ya awamu ya sita inatambua kuwa sekta ya utalii ina umuhimu katika ukuaji wa uchumi na maendeleo kwa ujumla. Katika kipindi cha mwaka 2021 - 2025 Mafanikio yaliyopatikana kutokana na ekta hii ni pamoja na:

(a)        Kuweka mazingira wezeshi na kuboresha miundombinu ya utalii;

(b)        Kubuni na kuanzisha vivutio vya utalii ikiwemo hifadhi ya Burigi-Chato;

(c)        Kusimamia rasilimali za misitu na nyuki minzinga 426,483.

 

Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi

Serikali imeendelea kutilia mkazo umuhimu wa maendeleo ya wananchi pamoja na ushirikishwaji wa makundi maalum ikiwemo vijana, wanawake na Watu Wenye Ulemavu ili kuleta usawa wa kijamii na kiuchumi kwa wote. Katika kufikia azma hiyo mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na:

(a)        Kuongezeka kwa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na Watu Wenye Ulemavu kutoka Shilingi bilioni 4,936,939,735.70 mwaka 2021 hadi Shilingi bilioni 8,659,406.081.40 za mwaka 2025; na

Kuendelea na utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF) ambapo jumla ya Shilingi bilioni 53,225,734,454 zilihawilishwa kwa kaya maskini 37,688, 

 (a)        kutekeleza miradi ya miundombinu 353 ya elimu, afya na barabara pamoja na kuwezesha walengwa kujiongezea kipato kupitia ufugaji na kilimo.

 

Michezo na Sanaa

Serikali inatambua kuwa sekta ya michezo na sanaa ina umuhimu mkubwa katika kutoa burudani, kuelimisha jamii, kuimarisha afya, kuunganisha jamii, kuzalisha ajira na kudumisha mila, tamaduni na desturi za kitanzania. Mkoa umeweza kuboresha miundombinu ya michezo na sanaa kwa lengo la kuimarisha udugu na umoja. Mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na:

(a)        Ujenzi wa viwanja vipya 2 vya mpira wa miguu ambavyo utekelezaji wake unaendelea; na

(b)        Kuhamasisha uanzishwaji wa vilabu vya michezo (ikiwemo Jogging).

 

Miradi ya Kimkakati

Serikali ya awamu ya sita imeendelea na kutekeleza miradi ya kimkakati kwa lengo la kuongeza mapato na kuwezesha utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na:

(a)        Kuendelea na ujenzi wa soko la samaki katika Halmashauri ya Chato;

(b)        Ujenzi wa miundombinu ya  stendi ya mabasi Chato yenye gharama ya shilingi bilioni 14 pamoja na stendi ya Bwanga;(a)        Kuendelea na ujenzi wa stendi na soko katika Halmashauri ya Bukombe yenye gharama ya Shilingi bilioni 16;

(b)        Kukamilika kwa machinjio ya kisasa katika eneo la mpomvu  Manispaa ya Geita;

(c)        Ujenzi wa soko la machinga-Katoro;

(d)        Kusimamia ujenzi wa mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (EACOP); na

(e)        Kuendelea na ujenzi wa uwanja wa mpira wa magogo katika Manispaa ya Geita wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 20,000 kwa gharama ya shilingi bilioni 2.1.

 

Utawala bora

Serikali ya awamu ya sita imejipambanua katika ujenzi wa demokrasia, utawala bora na utawala wa sheria ili kuwa na mazingira wezeshi kwa ajili ya ustawi wa jamii na maendeleo. Kuimarika kwa utawala bora kumewezesha kukuza demokrasia, kujenga moyo wa uzalendo, kudumisha amani na kuimarisha mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi. Mafanikio yaliyopatikana ni pamoja na:

(a)        Kukamilika kwa ujenzi wa Mahakama ikiwemo Mahakama za Wilaya ambapo mwaka 2021 kulikuwa na Mahakama 28 lakini hadi 2025 Mahakama zimeongezeka hadi 31;

(b)        Kuongezeka kwa vituo vya polisi kutoka 33 mwaka 2021 hadi vituo 38 mwaka 2025; na

Ujenzi wa majengo ya utawala 9, nyumba za viongozi 6 na za watumishi 24 katika Halmashauri za Nyang’hwale, Geita Manispaa, Bukombe, Halmashauri ya Geita, (a)        Mbogwe na katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita na Ofisi za Wakuu wa Wilaya za Nyang’hwale, Bukombe na Mbogwe.

 

HITIMISHO

Serikali ya awamu ya sita katika Mkoa wa Geita imejipanga kutekeleza Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025-2030 ili kufikia maleng ya Chama ya kuwahudumia wananchi katika nyanja zote za maisha.



 



Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

DUNIA NI KATILI SANA KWA MWANAUME MASIKINI

MWANAUME USIPITWE NA HILI, INASIKITISHA...?!!!

HUYU NDIYE MWANAMKE WA KUOA

DIARRA KIPA BORA TANZANIA

HATUNA TISHIO LA USALAMA MWANZA, HAKUNA WA KUJITANGAZIA JAMHURI YAO - RC MTANDA

CHINYELE ACHUKUA FOMU KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE DODOMA MJINI