ZAIDI YA SH. TRIL. 5 ZATUMIKA KATIKA MIRADI MBALIMBALI MWANZA


 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari MAELEZO jijini Dodoma Julai 16, 2025, kuhusu mafanikio ya mkoa huo katika miaka minne ya Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Waandishi wa Habari wakiwa katika mkoa huo.

Afisa Habari wa Idara ya Habari MAELEZO, Kelvin Kanje akiruhusu wanahabari kuuliza maswali.


1.0        MAFANIKIO KWA KILA SEKTA

Jumla ya Shilingi Trilioni 5.6 zimepokelewa Mkoani kipindi cha mwezi Novemba, 2020 hadi Aprili, 2025 kwa ajili ya maendeleo ya sekta mbalimbali kama ifuatavyo: -

 

1.1                 Sekta ya Afya

           Jumla ya Shilingi  Bilioni 63.2 zimetolewa

Mafanikio makubwa katika Sekta ya Afya ni wananchi kupata huduma kirahisi, kupunguza kusafirisha wagonjwa kwenda nje kwa kuendelea kupata huduma za kibingwa ambazo ni huduma za kibigwa za upasuaji, huduma za kibingwa za mifupa, huduma  za kibingwa za afya ya uzazi, huduma za kibingwa za sikio, pua na kinywa, huduma za kibingwa za magonjwa ya ndani pamoja huduma za kibingwa za saratani na huduma za kibingwa za magonjwa ya dharura. Yafuatayo yamemefanyika katika Kuboresha upatikanaji wa huduma hizo:-(i)   Ujenzi wa chanzo na Kituo cha Kusafisha na Kutibu Maji eneo la Butimba mradi umegharimu Shilingi. 71,696,910,869 na utazalisha lita 48,000,000 kwa siku. Hii itaboresha hali ya upatikanaji wa maji Mwanza. Kwa sasa miradi inayoendelea ni ya usambazaji maji kwenye maeneo yafuatayo:- Nyegezi, Mkolani, Butimba, Luchelele, Buhongwa, Igoma, Kisesa, Kishiri, Usagara  Nyashishi,  Mlima wa Rada, Nyamhongolo, Mnangani, Kambarage na Lwanhima na Sahwa,

(ii) Miradi ya ujenzi wa vyoo mashuleni na maeneo ya wazi yenye thamani ya Shilingi 7,492,265,910.54 imekamilika katika shule na vituo vya afya mbalimbali.

(iii)  Mradi wa uondoshaji maji taka katika maeneo ya milimani umetekelezwa kwa Shilingi 3,720,864,077.92 katika maeneo ya Pasiansi, Kilimahewa A, Kilimahewa B na Mabatini B. Ujenzi wa Mfumo wa Kutibu Majitaka katika Gereza Kuu la Butimba umegharimu Shilingi 1,969,862,600.

(iv)  Mradi wa upanuzi wa mabwawa ya majitaka kwa thamani ya Shilingi 6,739,048,681.80.

(v)   Visima vitano vya chanzo mbadala vimejengwa kwa Shilingi 294,844,126.00 na

(vi)  Wilaya ya Misungwi, MWAUWASA inaendelea kutekeleza mradi wa maji katika Kata ya Misungwi, Igokelo Iteja, Mwamanga, Mitindo B, Old Misungwi, Mbela B, C, D na Ng’ombe, na kunufaisha wakazi 22,482.

(vii)  Wilaya ya Ukerewe imepokea Shilingi 42,738,000.00 kwa ajili ya upanuzi wa miundombinu ya bomba katika maeneo ya Kakerege, Bugoye, Hamkoko Bulamba/Munfunzi na Namalebe ambapo wanufaika ni wananchi 3,500 na kaya 250.

 

c) Hali ya Upatikanaji wa Maji Safi Vijijini Mwaka 2020 hadi 2025

Kuanzia Julai 2020 hadi Mei 2025, imekamilisha jumla ya miradi 80 yenye thamani ya Shilingi 100,338,450,084.06 ambayo imepelekea hali ya upatikanaji wa maji vijijini kuimarika kwa kiwango kikubwa kutoka 57% 2021 hadi 77% mwaka 2025 kwa mchanganuo ufuatao:- Wilaya ya Kwimba imepanda kutoka 58% hadi 77.3%, Magu kutoka 44% hadi 73%, Misungwi kutoka 70.4% hadi 77.3%, Sengerema 57%  hadi 91% na Ukerewe  56% hadi 91%. Mafanikio hayo yametokana na utekelezaji wa miradi ifuatayo:-

(i)     Wilaya ya Kwimba imetekeleza miradi 29 ya maji katika vijiji mbalimbali pamoja na uchimbaji wa visima 22, Kwa gharama Shilingi. 22,046,262,574.43

(ii)   Wilaya ya Magu ilipokea Shilingi. 13,479,505,945.97 kwa utekelezaji wa miradi ya maji, uchimbaji wa visima 19 katika vijiji 5.

(iii)  Wilaya ya Misungwi ilipokea jumla ya Shilingi. 21,210,784,588, ambapo miradi ya thamani ya Shilingi. 7,122,836,106.08 imekamilika na ile ya Shilingi. 14,087,948,482.50 inaendelea kutekelezwa.

(iv)  Wilaya ya Sengerema imetekeleza miradi 27 ya maji yenye thamani ya Shilingi. 40,464,136,499.74 pamoja na uchimbaji wa visima 13.

(v) Ukerewe imetekeleza miradi 12 ya maji yenye thamani ya Shilingi. 15,277,263,613.41 katika maeneo ya Kazilankanda, Murutanga, Hamyebo na Busunda.

 

2.4        .Miundombinu ya Barabara

      Jumla ya Shilingi Bilioni 156.3 zimetolewa

Baadhi ya miradi iliyotekelezwa na TANROADS ya gharama ya Shilingi Bilioni 36.9 – kazi zinaendelea vizuri.

(i)           Jumla ya madaraja 13 yamekarabatiwa na kujengwa kwa gharama ya Shilingi Billioni 36.9 kwa mchanganuo ufuatao:

a)   Daraja la Simiyu linajengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 4.8

a)   Mkoa  una jumla ya hospitali za umma 10, Vituo vya afya 55 na zahanati 298. Hospitali za Wilaya zimeendelea kupatiwa fedha ili kuendelea na ujenzi mpaka sasa umegharimu jumla ya Shilingi 12,791,950,164.08

b)   Ukarabati wa hospitali za Wilaya ya Nyamagana, Magu na ukerewe kwa gharama ya Shilingi 5,171,802,836.30

c)   Ujenzi wa   Wodi ya Saratani, Jengo la Macho, uwekaji wa mitambo ya kufua Oksijeni na ukarabati wa ICU katika Hospitali ya  Rufaa ya Kanda Bugando kwa gharama ya Shilingi 9,872,000,000.

d)   Ujenzi wa Hospitali ya Ukerewe ambayo itakuwa yenye hadhi ya Rufaa ya Mkoa Shilingi 25,034,660,304.69 zimeletwa awamu ya kwanza inaendelea kujengwa katika kijiji cha Bulamba Wilaya ya Ukerewe.

e)   Idadi ya Wataalamu wa afya imeongezeka kutoka 2,855 mwaka 2020 hadi 4,150 mwaka 2025 sawa na ongezeko la wataalamu 1,295. Ajira mpya 1,015 na watumishi 280 wamehamia

f)     Idadi ya nyumba za watumishi zimeongezeka kutoka 355 mwaka 2020 hadi 436 mwaka 2025 sawa na ongezeko la nyumba 81

g)   Fedha zilizotengwa kwa ajili ya kununua dawa na vifaa tiba imeongezeka kutoka Shilingi 4,288,886,698.4 mwaka 2020/2021 hadi Shilingi 10,352,912,100.55 mwaka 2024/2025 sawa na ongezeko la Shilingi 6,064,025,332.15 a)   Upatikanaji dawa na vifaa tiba katika sehemu za kutolea huduma za afya umeongezeka kutoka asilimia 77.89 mwaka 2020 hadi asilimia 92.29 mwaka 2025 sawa na ongezeko la asilimia 14.73

b)   Idadi ya wananchi waliojiunga na Bima ya Afya iliyoboreshwa (Ichf) imeongezeka kutoka wananchi 294,304 mwaka 2020 hadi hadi 602,829 mwaka 2025 sawa na ongezeko la wananchi 308,647.

c)   Kiwango cha maambukizi ya malaria kimepungua kutoka asilimia 8 mwaka 2020 hadi asilimia 1 mwaka 2025.

d)   Huduma za upasuaji wa dharura vijijini zimeboreshwa kutoka vituo 17 mwaka 2020 hadi vituo 40 mwaka 2025 sawa na ongezeko la vituo 23

e)   Upatikanaji wa huduma za ubingwa na ubingwa Bobezi kwa kuleta  kambi za madaktari bingwa katika Mkoa kutoa huduma za kibingwa ambazo awali zilikuwa zikipatikana katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili pekee,

f)     Uwekaji wa mitambo ya kufua Oksijeni katika Sekou Toure umefanyika.

g)    Jumla ya maabara 3 zimepata ithibati (accreditation) zimefikia utambulisho wa ubora wa utoaji huduma za kimaabara ngazi ya Kimataifa ambazo ni maabara iliyopo Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou Toure, Hospitali ya Nyamagana na Sengerema DDH.

h)   Huduma ya uchunguzi kwa kipimo cha Utrasound imeboreshwa kutoka vituo 2 mwaka 2020 hadi vituo 45 mwaka 2025.

a)   Upatikanaji dawa na vifaa tiba katika sehemu za kutolea huduma za afya umeongezeka kutoka asilimia 77.89 mwaka 2020 hadi asilimia 92.29 mwaka 2025 sawa na ongezeko la asilimia 14.73

b)   Idadi ya wananchi waliojiunga na Bima ya Afya iliyoboreshwa (Ichf) imeongezeka kutoka wananchi 294,304 mwaka 2020 hadi hadi 602,829 mwaka 2025 sawa na ongezeko la wananchi 308,647.

c)   Kiwango cha maambukizi ya malaria kimepungua kutoka asilimia 8 mwaka 2020 hadi asilimia 1 mwaka 2025.

d)   Huduma za upasuaji wa dharura vijijini zimeboreshwa kutoka vituo 17 mwaka 2020 hadi vituo 40 mwaka 2025 sawa na ongezeko la vituo 23

e)   Upatikanaji wa huduma za ubingwa na ubingwa Bobezi kwa kuleta  kambi za madaktari bingwa katika Mkoa kutoa huduma za kibingwa ambazo awali zilikuwa zikipatikana katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili pekee,

f)     Uwekaji wa mitambo ya kufua Oksijeni katika Sekou Toure umefanyika.

g)    Jumla ya maabara 3 zimepata ithibati (accreditation) zimefikia utambulisho wa ubora wa utoaji huduma za kimaabara ngazi ya Kimataifa ambazo ni maabara iliyopo Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Sekou Toure, Hospitali ya Nyamagana na Sengerema DDH.

h)   Huduma ya uchunguzi kwa kipimo cha Utrasound imeboreshwa kutoka vituo 2 mwaka 2020 hadi vituo 45 mwaka 2025.

a)   Digital X- ray zimeongezeka kutoka 2 mwaka 2020 hadi  26 mwaka 2025. (Nyamagana 5, Ilemela 4 Kwimba 3, Misungwi 4, Sengerema 3, Magu 3, Ukerewe 4) 

b)   Jumla ya CT Scan 3 zimenunuliwa zimeanza kutoa huduma katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda – Bugando, Hospitali ya Mkoa Seko Toure na Hospitali ya Jeshi.

c)   Mashine ya MRI imenunuliwa na Serikali na imesimikwa katika Hospitali ya  Rufaa ya Kanda Bugando.

 

2.2    Sekta ya Elimu

    Jumla ya Shilingi  Bilioni  196.8 zimetolewa

Miundombinu  imeboreshwa  ambayo imesaidia  kumepunguza kwa kiasi kikubwa umbali wa kutembea kwenda shule, msongamano wa wanafunzi madarasani, kuwezesha mazingira bora zaidi kwa walimu na wanafunzi. Maboresho yafuatayo  yamefanyika  :-

(i)   Mpango wa Elimu Bila Malipo kwa shule za msingi katika Mkoa umegharimu jumla ya Shilingi 32,812,096,940.45 kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi 2024/2025. Utekelezaji wa mpango huu umewezesha uboreshaji wa mazingira ya kujifunzia na kufundishia, sambamba na kuhakikisha upatikanaji wa elimu bora, jumuishi na isiyo na vikwazo vya ada kwa wanafunzi

(ii) Mpango wa Elimu Bila Malipo kwa shule za sekondari umegharimu jumla ya Shilingi 44,695,682,656.24 kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi 2024/2025.

(iii)  Idadi ya shule za msingi imeongezeka kutoka shule 873 mwaka 2020 hadi shule 930 mwaka 2025, sawa na ongezeko la shule 57.

(iv)  Idadi ya shule za sekondari imeongezeka kutoka shule 219 mwaka 2020 hadi shule 308 mwaka 2025, sawa na ongezeko la shule 89.

(i)     Idadi ya vyumba vya madarasa katika shule za msingi imeongezeka kutoka vyumba 7,464 mwaka 2020 hadi kufikia vyumba 8,866 mwaka 2025, sawa na ongezeko la vyumba 1,402.

(ii)   Idadi ya vyumba vya madarasa katika shule za sekondari imeongezeka kutoka vyumba 3,175 mwaka 2020 hadi 5,742 mwaka 2025, sawa na ongezeko la vyumba 2,567.

(iii)    Idadi ya vyumba vya maabara katika shule za sekondari imeongezeka kutoka vyumba 421 mwaka 2020 hadi vyumba 579 mwaka 2025, sawa na ongezeko la vyumba 158.

(iv)    Idadi ya matundu ya vyoo katika shule za msingi imeongezeka kutoka 10,202 mwaka 2020 hadi 13,423 mwaka 2025, sawa na ongezeko la matundu 3,221.

(v)     Idadi ya matundu ya vyoo katika shule za sekondari imeongezeka kutoka 3,903 mwaka 2020 hadi 5,901 mwaka 2025, sawa na ongezeko la matundu 1,998.

(vi)    Jumla ya vifaa 243 vya TEHAMA vimewekwa katika shule za sekondari kwa gharama ya jumla ya Shilingi 241,250,000.00 kwa lengo la kuboresha mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Utekelezaji huu umewezesha wanafunzi kupata fursa ya kutumia vifaa vya kidijitali katika kukuza maarifa, kuongeza ufanisi wa ujifunzaji wa masomo ya sayansi, hisabati, na stadi za maisha, sambamba na kuimarisha ujuzi wa TEHAMA miongoni mwa walimu na wanafunzi.

(vii)Idadi ya mabweni imeongezeka kutoka mabweni 61 mwaka 2020 hadi mabweni 184 mwaka 2025, sawa na ongezeko la mabweni 123.

(viii) Idadi ya mabweni ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika shule za msingi imeongezeka kutoka mabweni 0 mwaka 2020 hadi mabweni 4 mwaka 2025, sawa na ongezeko la mabweni 4.(i)       Idadi ya mabwalo ya kulia chakula katika katika shule za sekondari  imeongezeka kutoka mabwalo 14 mwaka 2020 hadi mabwalo 21 mwaka 2025, sawa na ongezeko la mabwalo 7.

(ii)     Ujenzi wa Chuo cha Uhasibu cha TIA – Kampasi ya Mwanza umekamilika kwa gharama ya Shilingi 9,800,000,000

(iii)    Ujenzi wa vyuo vitatu vya ufundi (VETA) katika Halmashauri za Magu, Misungwi na Buchosa unaendelea kwa gharama ya Shilingi 10,200,000,000 kwa lengo la kuimarisha elimu ya ufundi stadi kwa vijana na kuwawezesha kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi.  Ujenzi unaendelea.

(iv)      Ujenzi wa chuo cha ufundi kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum katika Halmashauri ya Magu unaendelea na umefikia hatua za ukamilishaji.

(v)       Ujenzi wa miundombinu katika Chuo cha Michezo Malya kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba kwa gharama ya Shilingi 34,082,032,000 unaendelea.

(vi)      Ujenzi wa Maktaba  ya Mkoa kwa gharama ya Shilingi 2,887,000,000 unaendelea

(vii)  Ujenzi wa Chuo cha Dar es salaam Institute of Techology (DIT) – Kampasi ya Mwanza kwa gharam ya Shilingi 26,843,347,993 unaendelea.

(viii)   Ujenzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) – Kampasi ya Mwanza kwa gharama ya Shilingi 5,365,840,722  unaendelea.

Uandikishaji wanafunzi elimu ya awali umeongezeka kutoka wanafunzi 134,626 mwaka 2020 hadi wanafunzi 592,177 mwaka 2025. Darasa la Kwanza umeongezeka kutoka wanafunzi 163,723 mwaka 2020 hadi wanafunzi 711,107 mwaka 2025, sawa na ongezeko la wanafunzi 547,384, Kidato cha Kwanza umeongezeka kutoka 

(i)         wanafunzi 63,392 mwaka 2020 hadi wanafunzi 324,346 mwaka 2025, ikiwa ni ongezeko la wanafunzi 260,954, Kidato cha Tano umeongezeka kutoka wanafunzi 11,719 mwaka 2020 hadi kufikia wanafunzi 82,969 mwaka 2024, sawa na ongezeko la wanafunzi 71,250.

(ii)       Ufaulu wa mitihani Kidato cha Pili umeongezeka kutoka asilimia 91.5 mwaka 2020 hadi asilimia 97.1 mwaka 2025 kwa mkoa mzima wa Mwanza, sawa na ongezeko la wastani la asilimia 5.6.  Kidato cha Nne umeongezeka kutoka asilimia 88.37 mwaka 2021 hadi asilimia 96.34 mwaka 2024, sawa na ongezeko la wastani wa asilimia 7.97. Kidato cha Sita katika Mkoa umeongezeka kutoka asilimia 97.62 mwaka 2021 hadi asilimia 99.76 mwaka 2024, sawa na ongezeko la wastani wa asilimia 2.14.

(iii)          Idadi ya walimu wa shule za msingi imeongezeka kutoka walimu 11,915 mwaka 2020 hadi walimu 12,977 mwaka 2025, sawa na ongezeko la walimu 1,062.

(iv)          Idadi ya walimu wa shule za sekondari imeongezeka kutoka walimu 5,675 mwaka 2020 hadi kufikia walimu 6,715 mwaka 2025, sawa na ongezeko la walimu 1,040.

(v)         Jumla ya wanafunzi wa kike 485 walioacha shule wamepata nafasi ya kurudi shule.

 

2.3    Sekta ya Huduma ya Maji Mijini na Vijijini

          Jumla ya Shilingi Bilioni 264.8 zimetolewa

 

a)       Hali ya upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama imeongezeka:

§   Mijini, kutoka 57% hadi 85%

§   Vijijini, kutoka 57% hadi 77.8%

 

b)       Hali ya upatikanaji maji mijini (MWAUWASA)

Kuanzia Julai 2020 hadi Mei 2025, jumla ya miradi 19 yenye thamani ya Shilingi 164,419,664,492.55 imekamilika kwa kutekeleza yafuayao:-a)   Daraja la Sukuma: linajengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 9.4

b)   Daraja la Mabatini: linajengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 6

c)   Daraja la Mkuyuni: linajengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 5.2

d)   Daraja la Nyaluha na Kishinda: Mradi huu unatekelezwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 3.3

e)   Daraja la Sakanti na Malemve: mradi huu unatekelezwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 5.5

f)     Jumla ya madaraja 7 madogo yamejengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1.6 katika Halmashauri za Wilaya ya Ilemela, Magu, Kwimba na Buchosa

g)   Jumla ya Makalavati 143 yamejengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 1 katika Mkoa wa Mwanza

h)   Jumla ya madrift 2 yamejengwa kwa gharama za Shilingi Millioni 100 katika Halmashauri ya Buchosa

i)     Jumla ya taa 1,374 zimewekwa katika Mkoa wa Mwanza.

 

ii) Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA)

Baadhi ya miradi mikubwa ya barabara iliyotekelezwa na TARURA ya gharama ya Shilingi Bilioni 72.7– kazi zinaendelea vizuri.

a)   Mtandao wa barabara za lami umeongezeka kutoka Km 76.82    mwaka 2020 hadi Km 103.08 mwaka 2025 sawa na Ongezeko la Km 26.26.

b)   Mtandao wa barabara za mawe umeongezeka kutoka Km 14.75  mwaka 2020 hadi Km 21.14  mwaka 2025 sawa na ongezeko la Km 6.29.

c)   Mtandao wa barabara za changarawe umeongezeka kutoka Km 2375.352 mwaka 2020 hadi Km 3996.442 mwaka 2025 sawa na ongezeko la Km  1621.a)   Ujenzi wa barabara  ya Buhongwa – Igoma kiwango cha Lami yenye urefu wa Km 14.4 utekelezaji umefikia 66.67%

b)   Ujenzi wa barabara ya Buswelu – Nyamadoke -  Nyamhongolo kiwango cha lami Km  9.5 ujenzi unaendelea.

c)   Ujenzi wa barabara ya  Buswelu – Busenga – Coca cola  kwango cha lami Km 3.3 ujenzi unaendelea

d)   Ujenzi wa barabara  ya Majengo kiwango cha lami yenye urefu wa Km 0.5 ujenzi unaendelea.

e)   Matengenezo ya barabara ya Kanyerere – Gabajiga - Budutwa kwa kiwango cha lami Km  9.9 kazi inaendelea

 

2.4        Uboreshaji Bandari (Mwanza Kaskazini)

 Jumla ya Shilingi Bilioni 18.6 zimetolewa

Uboreshaji unahusisha majengo ya abiria ili kuhudumia abiria wengi zaidi, kuongeza eneo la maegesho ya magari, kuongeza urefu wa gati na kina cha maji. Ujenzi wa uzio, taa na kamera za usalama ujenzi za mto mirongo katika eneo la bandari Utekelezaji, bandari na 58%.

 

2.5        Ujenzi wa Vivuko 

     Jumla ya Shilingi 18,674,414,228.51 zimetolewa

Mradi wa ujenzi wa vivuko vipya vitano (5) vya Kisorya – Rugenzi Wilaya ya Ukerewe -  chenye thamani ya Shilingi 892,760,706.00 Ijinga – Kahangala 5,255,080,099.51 – Magu,  Bwiro – Bukondo Shilingi 676,164,840.00 - Ukerewe  Nyakarilo – Kome Shilingi 8,033,344,250.00 - Buchosa,  Buyagu - Mbalika Shilingi 3,817,064,333.00 unaendelea.- Misungwi. Vivuko 12 vilivyopo vimeendelea kufanyiwa ukarabati  ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

2.6            Usafiri wa anga umeboreshwa

   Jumla ya Shilingi. 34,515,699,054.21 zimetolewa a)   Ujenzi wa Jengo Jipya la Abiria (New Terminal Building) Jengo hili lenye uwezo wa kuhudumia abiria 400,000 kwa mwaka, kwa fedha za kitanzania Shilingi 29,320,221,747.33 ujenzi unaendelea.

b)   Jumla ya Shilingi 5,195,477,306.88  zimetolewa kwa ajili ya kuboresha uwanja wa ndege kwa  maandalizi ya kuwa uwanja wa kimataifa shughuli zifuatazo zimetekelezwa:- Ujenzi wa Uzio wa ndani wa Usalama (Inner Security Fence) wa km 12, mageti 13, ujenzi wa makalavati ya urefu wa mita 15 kuzunguka uwanja, Ujenzi wa Mfumo wa tozo za maegesho ya magari (electronic car parking management System), kuweka mfumo wa kisasa wa kuhudumia mizigo, utengenezaji wa “Runway Designation Markings”,Ujenzi wa Uzio wa Usalama (Security Fence) katika Ofisi za Utawala na ukarabati wa Jengo la Zimamoto

2.4           Usafiri wa majini

Jumla ya Shilingi biilioni 156.9 zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa meli mpya na ukarabati

a)   Mradi wa ujenzi wa meli mpya ya “MV Mwanza Hapa kazi Tu” kwa gharama ya Shilingi 120,6. Meli hii itakuwa na uwezo wa kubeba abiria 1,200, tani 400 za mizigo, magari madogo 20 na malori 3. Mradi huu utekelezaji wake umefikia asilimia 96

b)   Mradi wa ukarabati wa meli  ya uokozi (Tug boat) ya MT Ukerewe na MV Umoja Kazi iendelee  kwa gharama ya Shilingi  26.9. Ukarabati umekamilika

c)   Ununuzi wa Boti za Utafutaji na Uokozi pamoja na boti ya matibabu Kwa gharama ya Shilingi Billioni 4.5 ujenzi umekamilika

Ujenzi wa Kituo cha Kikanda cha Kuratibu Utafutaji na Uokozi (Zonal Maritime Search and Rescue a)   Coordination Centre) Ilemela Mwanza kwa gharama Shilingi Billioni 4.9 ujenzi umefikia asilimia 90.

2.4           Nishati ya Umeme

          Jumla ya Shilingi 110,104,728,354.78 zimetolewa

     Umeme katika Vijiji na Vitongoji: -

(i)     Vijiji 522 vya nchi kavu vimeunganishwa umeme kwa asilimia 100, Vijiji 23 ambavyo ni visiwa viko kwenye mpango wa mradi wa nishati ya jua kwa kaya binafsi.

(ii)   Vitongoji 1,808 kati ya 3,448 vimeungwa umeme sawa na 52%.

(iii)  REA imetumia Shilingi 94,280,441,937.14 katika miradi mbalimbali ya usambazaji umeme vijijini.

(iv)  Miradi ya PERI-URBAN kwa Shilingi 9,943,685,936.05

(v)   Mradi wa kupeleka umeme kwenye vyanzo vya maji  kwa gharama ya Shilingi 4,111,334,164

(vi)  Mradi wa kupeleka umeme kwa wachimbaji wadogo kwa gharama ya Shilingi 1,769,266,317.59

(vii)  Jumla ya taasisi za umma 32 zimehamasishwa kutumia nishati mbadala ya kupikia ya gasi

(viii)   Jumla ya majiko ya gasi 25,235 yameuzwa kwa wananchi  kwa bei ya ruzuku

 

 

2.5        Sekta ya Kilimo

a)   Uzalishaji wa mazao ya chakula umeongezeka kutoka tani 640,205.3 (37.59%) 2020/21 hadi kufikia tani 1,025,784.08 (60.23%) mwaka 2024/25 sawa na ongezeko la Tani 385,578 (22.64%)

b)   Ujenzi na ukarabati wa miradi ya umwagiliaji 2 ya Sengerema Katunguru na Mahiga kwimba kwa gharama ya Shilingi. 54,473,623,973.41 unaendelea Upatikanaji wa viuatilifu umeongezeka kutoka chupa 324,821 Mwaka 2020 hadi chupa 832499 Mwaka 2025.a)   Upatikanaji wa mbolea Ruzuku umeongezeka kutoka tani 249.4 Mwaka 2020 hadi 3,611.25 mwaka 2025 sawa na ongezeko la tani 3,361.8.

b)   Katika kuboresha maslahi ya wakulima, mfumo wa kununua mazao kupitia vyama vya Ushirika vya Msingi (AMCOS) vimeongezeka kutoka vyama 164 mwaka 2018 hadi vyama 257 mwaka 2025.

c)   Vitendea kazi vimetolewa kwa maafisa ugani. Idadi ya vishikwambi imeongezeka kutoka vishikwambi 29 Mwaka 2020 hadi vishikwambi 272 mwaka 2025, Idadi ya pikipiki imeongezeka kutoka pikipiki 42 mwaka 2020 hadi pikipiki 256 mwaka 2025 jumla ya Vifaa vya kupima udongo 15 vimetolewa

 

 

2.4        Sekta ya Mifugo

a)   Uzalishaji wa mitamba umeongezeka kutoka mitamba 58,625 mwaka 2020 hadi 215,775 mwaka 2025 sawa na ongezeko la mitamba 157,149.

b)   Mauzo ya mitamba kwa wananchi yameongezeka kutoka mitamba 44,320 mwaka 2020 hadi mitamba 143,926 mwaka 2025 sawa na ongezeko la mauzo ya mitamba 99,606.

c)   Idadi ya majosho mapya yaliyojengwa mwaka 2020 yalikuwa 55 yameongezeka hadi kufikia majosho mapya 76 mwaka 2025  sawa na ongezeko la majosho 21.

d)   Idadi ya viwanda vya nyama na mazao mengine ya mifugo vilivyoanzishwa imeongezeka kutoka viwanda 3 mwaka 2020 hadi 6 mwaka 2025 sawa na ongezeko la viwanda 3.

e)   Idadi ya mabwawa ya kunyweshea mifugo yamejengwa kutoka mabwawa 121 mwaka 2020 hadi mabwawa 238 mwaka 2025 sawa na ongezeko la mabwawa 117.2.4        Sekta ya Uvuvi

a)   Ufugaji wa samaki kwa kutumia njia ya kisasa umeongezeka kutoka vizimba (fish cauges) 1,664 mwaka 2020 hadi 2,715 mwaka 2025 sawa na ongezeko la vizimba 1,051.

b)   Jumla ya tani 43,657.6 za minofu ya Samaki zimechakatwa na tani 81,812 zimesafirishwa kwenda soko la nje ya Nchi kupitia Uwanja wa Ndege wa Mwanza kwa kipindi cha mwaka 2024

c)   Kilo za mabondo zilizosafirishwa kwenda soko la nje ya Nchi kupitia Uwanja wa Ndege wa Mwanza zimeongezeka kutoka kilo 431,721 mwaka 2020 hadi kilo 495,448 mwaka 2024 sawa na ongezeko la kilo 63,727.

d)   Idadi ya mabwawa ya ufugaji wa Samaki imeongezeka kutoka 286 mwaka 2020 hadi mabwawa 531 mwaka 2025 sawa na ongezeko la mabwawa 245.

e)   Kiasi cha mapato yaliyotokana na shughuli za uvuvi kimeongezeka kutoka Shilingi 4,416,172,821.59 mwaka 2020 hadi Shilingi 8,233,724,351.33 mwaka 2025 sawa na ongezeko la Shilingi 3,817,551,529.74.

 

2.5        Mazingira, Maliasili na Utalii

a)   Idadi ya watalii waliotembelea Hifadhi ya Taifa ya Saanane imeongezeka kutoka 13,175 mwaka 2020 hadi 24,748 mwaka 2025 sawa na ongezeko la watalii 11,573.

b)   Mapato ya Hifadhi ya Taifa ya Saanane yatokanayo na Utalii yameongezeka kutoka Shilingi 210,818,714.53 mwaka 2020 hadi Shilingi 274,488,877.09 mwaka 2025 sawa na ongezeko la Shilingi 63,670,162.56

 

2.6        Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Biashara na Uwekezaji

a)        Jumla ya Shilingi Bilioni 85.8 zimewezesha Wananchi Kiuchumi

§   Vikundi vya wanawake, vijana na wenye ulemavu vilivyopewa mikopo ya asilimia 10 isiyo na riba vimeongezeka kutoka 630 hadi 1,856. Aidha, kiwango cha mikopo iliyotolewa nacho kimeongezeka kutoka Shilingi Bilioni 3.3 hadi Shilingi. Bilioni 14.1.

§   Kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF), Jumla ya kaya 59,932 zimenufaika Shilingi Bilioni 44 zimetolewa kwa walengwa.

§   Mifuko mingine iliyowezesha wananchi ni pamoja na  Mfuko wa Taifa wa Kuendeleza Wajasiriamali Wananchi (National Entrepreneurship Development Fund) umetoa mikopo ya Shilingi. 371,000,000 kwa wanaufaika 160, Mfuko wa Mzunguko wa Mikoani (SIDO RRF); umetoa mikopo kwa vijana 38 yenye thamani ya Shilingi 26,000,000. Mfuko wa Kutoa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo (SELF Microfinance Fund); jumla Shilingi. 27,369,130,990 zimetolewa kwa wanaufaika 173,6000.

a)        Biashara na Uwekezaji

§   Katika Mkoa wa Mwanza Idadi ya Viwanda Vikubwa   imeongezeka kutoka 46 mwaka 2020 hadi viwanda 50 mwaka 2025 sawa na ongezeko la viwanda 4.

§   Idadi ya viwanda vya kati imeongezeka kutoka 109 mwaka 2020 hadi viwanda 116 mwaka 2025 sawa na ongezeko la viwanda 7.

§   Idadi ya viwanda vidogo na vidogo sana imeongezeka kutoka  viwanda 1,776 mwaka 2020 hadi viwanda  2,322 kwa Mwaka 2025 sawa na ongezeko la viwanda 546.

§    Idadi ya biashara zenye leseni imeongezeka kutoka 23,704 mwaka 2020 hadi 29,606 mwaka 2025 sawa na ongezeko la biashara zenye leseni 5,902.

 

2.4            Ukusanyaji Mapato ya Ndani katika Halmashauri

Makusanyo yameongezeka kutoka jumla ya Shilingi Bilioni 44.2 mwaka 2020/21 hadi Shilingi Bilioni 70.7 mwaka 2024/25 kufikia mwezi Mei, 2025 sawa na ongezeko la 60%. Aidha, kwa kipindi cha miaka mitano (5) zimekusanywa jumla ya Shilingi Bilioni 216.2

 

2.4            Utekelezaji wa Miradi ya Kimkakati Kuchachua Uchumi wa Mkoa

Mkoa umeendelea kutekeleza Miradi mbalimbali ya Kimkakati kwa gharama ya Shilingi 3,969,880,676,469.24 Kwa mchanganuo ufuatao:-

a)   Ujenzi wa Reli SGR Mwanza - Isaka kwa  Shilingi 3,062,031,806,702.83, unaendelea

b)   Ujenzi wa Daraja la JPM Kigongo - Busisi kwa Shilingi 716,333,000,000.0 umekamilika.

c)   Ujenzi wa Meli Mpya ya MV MWANZA kwa gharama ya Shilingi 120,562,787,135.31, unaendelea

d)   Ujenzi wa kituo cha Mabasi Nyegezi kwa gharama ya Shilingi      18,750,376,421.33 umekamilika

e)   Ujenzi wa kituo cha Mabasi na Malori Nyamhongolo kwa gharama ya Shilingi 24,197,267,650.77 umekamilika

f)     Ujenzi wa Soko Kuu Mwanza kwa gharama ya Shilingi 26,605,438,559.00 umekamilika

2.5            Utawala Bora na Uboreshaji wa Mazingira ya Kufanyia Kazi

a)   Jumla ya watumishi 4,970 wameajiriwa katika kipindi cha mwaka 2020 – 2025  kwa ajili ya kuboresha huduma kwa wananchi.

b)   Idadi ya nyumba 6 za wakurugenzi zimejengwa kwa kipindi cha  kuanzia mwaka 2020 – 2025 

c)   Idadi ya nyumba 4 za wakuu wa wilaya zimejengwa kuanzia mwaka 2020 – 2025 

d)   Idadi ya nyumba 4 za makatibu tawala  wa wilaya zimejengwa kuanzia mwaka 2020 – 2025  a)   Jumla ya nyumba 143 za watumishi zimejengwa kuanzia mwaka 2020 – 2025 

b)   Idadi ya Ofisi za watendaji wa kata zimeongezeka kutoka ofisi 96 mwaka 2020 hadi ofisi 113 mwaka 2025 sawa na ongezeko la ofisi 17.

c)   Ujenzi wa majengo ya utawala yameongezeka kutoka majengo 2 mwaka 2020 hadi majengo 8 mwaka 2025 sawa na ongezeko la majengo ya utawala 6

d)   Idadi ya nyumba za wakuu wa Idara zimeongezeka kutoka nyumba 5 mwaka 2020 hadi nyumba 24 mwaka 2025 sawa na ongezeko la nyumba 19

e)   Idadi ya magari kwa ajili ya matumizi ya ofisi imeongezeka kutoka magari 147 mwaka 2020 hadi magari 184 mwaka 2025 sawa na ongezeko la magari 37

f)     Idadi ya ofisi za maafisa tarafa zimeongezeka kutoka 3 mwaka 2020 hadi 15 mwaka 2025 sawa na ongezeko la ofisi 12

g)   Jumla ya watumishi 25,934 wamepandishwa madaraja 

h)   Jumla ya watumishi 19,722 wamepandwa Vyeo

i)     Jumla ya watumishi 4,068 wamelipwa madeni yasiyo ya mishahara yenye thamani ya Shilingi 3,849,275,634.54

 

HITIMISHO

Mkoa wa Mwanza unaipongeza sana Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuleta maendeleo katika Taifa letu. Mkoa unaahidi kutoa ushirikiano katika kufanikisha maendeleo ya uchumi ili kuwezesha kutoa huduma zilizo bora kwa wananchi. Kwa niaba ya wananchi  wa Mkoa wa Mwanza tunamtakia Mhe. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kheri na baraka katika kusimamia utendaji wa shughuli za Serikali kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo ya haraka.

 

                                                           

 

 

 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

DUNIA NI KATILI SANA KWA MWANAUME MASIKINI

MWANAUME USIPITWE NA HILI, INASIKITISHA...?!!!

DIARRA KIPA BORA TANZANIA

MAKUNDI YA VILABU VINAVYOSHIRIKI KOMBE LA DUNIA 2025.

HUYU NDIYE MWANAMKE WA KUOA

CHINYELE ACHUKUA FOMU KUOMBA RIDHAA YA KUGOMBEA UBUNGE DODOMA MJINI