Jana, Prof Sospeter Muhongo alipiga Kampeni kwenye vijiji viwili (Chimati & Chitare) vya Kata ya Makojo.
Vijiji hivi tayari vimefikishiwa umeme na maji ya bomba kutoka Ziwa Victoria. Usambazaji unaendelea kwenye ngazi ya vitongoji.
Kwa maendeleo yaliyokwishapatikana, vijiji hivi vimeamua kutoa kura nyingi sana kwa wagombea wote wa CCM, wakiongozwa na Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
Hamasa: tafadhali sikiliza muziki (Video/Clip iliyoambatanishwa hapa) utokao kwenye gita za zamani za Wanamuziki wa Kijijini Chimati.
Kamati ya Uchaguzi
Jimbo la Musoma Vijijini
Wed, 17 Sept 2025
Comments