SINGIDA ILIVYOITIKA KAMPENI ZA DKT. SAMIA






Sehemu ya umati wa wanachama, wapenzi na wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwenye Uwanja wa Bombadia Mjini Singida leo Septemba 9, 2025.katika Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais Kupitia CCM, Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi wa Singida katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa Chama hicho zilizofanyika katika uwanja wa Bombadia mkoani Singida tarehe 09 Septemba, 2025.


Pamoja na mambo mengine, Dkt.Samia amewaahidi wakazi wa Mkoa wa Singida kuwatafutia soko la mazao ya jamii ya mikunde ambayo ni dengu na mbaazi ili wakulima hao waweze kunufaika na zao hilo kwa kuuza bei yenye faida.


Dkt. Samia amesema serikali ipo kwenye mazungumzo na serikali ya India ili kutafuta soko hilo ambapo amewahakikishia wakulima kuwa makubaliano yatakayofanyika hayatoshuka chini ya asilimia 60 ya soko la dunia.


> Vilevile, amewaasa wakulima hao kutokuuza mazao hayo akiwaahidi hivi karibuni serikali ina mpango wa kutoa vibali kwa wafanyabishara kusafirisha mazao hayo nje ya nchi.


> Dkt. Samia amesema hayo leo Septemba, 2025 mkoani Singida wakati wa mkutano wake wa kampeni

Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM, ambaye ni Mratibu wa kampeni za chama hicho Kanda ya Kati mikoa ya Dodoma, Singida na Tabora akizungumza wakati wa mkutano huo, ambapo amemsifia Dkt. Samia kuwa ni mgombea bora kutoka chama bora na anafaa kuendelea kuongoza Nchi kwa miaka mingine mitano.

Pia amewajengea wanawake ujasiri wa kujiamini ndiyo maana wanashika nafasi za juu za uongozi.
Matukio mbalimbali katika mkutano wa hadhara wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika katika uwanja wa Bombadia mkoani Singida tarehe 09 Septemba, 2025.

Waendesha baiskeli wakioongoza msafara wa Dkt. Samia kuingia kwenye Uwanja wa Bombadia.

Nishangwe kwa kwenda mbele.







 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

NENO KUNTU LA UMMY MWALIMU ALILOLITOA BAADA YA KUTEMWA KUGOMBEA UBUNGE

WAGOMBEA WALIOENGULIWA CCM LICHA YA KUONGOZA KURA ZA MAONI

CHONGOLO AMKUMBUKA DKT. ASHA-ROSE MIGIRO-

RC KIHONGOSI AELEZA MAFANIKIO LUKUKI MKOA ARUSHA

MBINU ZITAKAZOKUFANYA USIISHIWE PESA