OSIMHEN HATOMSAHAU BACCA

 


LICHA ya Taifa Stars kupoteza kwa bao 2-1 dhidi ya Nigeria, beki wa Stars, Ibrahim Bacca ameonesha kiwango cha juu kwa kumdhibiti vyema mshambuliaji hatari wa Nigeria na klabu ya Galatasaray, Victor Osimhen.


Katika mchezo huo, Osimhen alionekana kukosa nafasi nyingi alizotarajia, huku akionesha dalili za kutofurahia kufanyiwa mabadiliko kabla ya kumalizika kwa dakika 90 bila mafanikio yoyote mbele ya lango la Stars.


Ulinzi wa Taifa Stars ulisimama imara kwa nyakati nyingi, jambo linaloonesha maendeleo makubwa ya timu licha ya matokeo.


Vipi wewe mdau wa soka, umeonaje kiwango cha Taifa Stars katika mchezo huu?


Timu ya Taifa ya Tanzania imepoteza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Nigeria kwa bao 2-1  katika mashindano ya AFCON 2025 yanayofanyika Nchini Morocco.


Katika mchezo huo Nigeria walikuwa wakwanza kupata goli kupitia kwa Beki wao wa kati mnamo dakika ya 36 Semi Ajayi, Stars ikasawazisha bao Hilo dakika ya 50 ya mchezo kupitia Charles M'mombwa, dakika ya 52 Adebora Lookman akaiandikia Nigeria bao la 2 na kufanya mchezo huo kumalizika kwa bao 2-1.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

UKWELI KUHUSU TENDO LA NDOA NA FAIDA ZAKE

MAPACHA WATATU FAMILIA YA MWAIKENDA WAPATA KIPAIMARA

๐Œ๐‰๐”๐„ ๐Š๐€๐‚๐‡๐„๐‘๐Ž ๐Œ๐™๐„๐๐€

NAMNA YA KUTENGENEZA MAISHA YAKO KIMYA KIMYA

VITU 10 WANAUME WANAVYOPENDA ZAIDI TOKA KWA MWANAMKE — SIYO SURA, SIYO MWILI ❤️

Wasifu wa Kizza Besigye

NAPE AWAPA UKWELI VIJANA

USIKUBALI KUWA LOFA KWA MWANAMKE...