RAIS WA SENEGAL ATAMGAZA LIKIZO KUSHEREHEKEA UBINGWA WA KOMBE LA AFRIKA

Rais wa Senegal atangaza likizo ya kitaifa kufuatia ubingwa wa Kombe la Afrika.

Rais wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, ametangaza kuwa leo ni siku ya mapumziko ya kitaifa ili kuwapa wananchi wa Senegal fursa ya kutosha kusherehekea ushindi wa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) walioupata usiku uliopita.

Kupitia taarifa rasmi, Rais Faye amesema uamuzi huo unalenga kuunga mkono furaha ya wananchi na kuimarisha mshikamano wa kitaifa baada ya mafanikio makubwa ya timu ya taifa. Alisisitiza kuwa ushindi huo ni fahari kwa taifa zima na ni matokeo ya juhudi, nidhamu na mshikamano wa Wachezaji pamoja na sapoti ya wananchi.

Akizungumza kuhusu maamuzi hayo, Rais Faye alinukuliwa akisema, “Nimetangaza siku ya leo kuwa ni likizo ya kitaifa ili wananchi wa Senegal wapate muda wa kutosha kusherehekea ushindi wa Kombe la Afrika tulilolinyakua usiku uliopita.”

Tangazo hilo limepokelewa kwa shangwe kubwa nchini kote, ambapo wananchi wanatarajiwa kujitokeza kwa wingi katika maeneo mbalimbali kushiriki shamrashamra za ushindi huo wa kihistoria. Serikali imewahimiza wananchi kusherehekea kwa amani na kuzingatia usalama, huku ikitambua mchango wa kila mmoja katika safari ya mafanikio ya taifa hilo kwenye soka la Afrika.

Toa maoni yako



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

MAPACHA WATATU FAMILIA YA MWAIKENDA WAPATA KIPAIMARA

MVUA KUBWA KUNYESHA MIKOA 20

AINA 4 ZA WANAWAKE WASIOWEZA KUDUMISHA NDOA.

MIKOA 10 YENYE KIPATO KIKUBWA ZAIDI KWA MTU MMOJA MMOJA

BODABODA ALIPWA PIKIPIKI BAADA KUSAFIRI KWA BODA KWA SAA 10 MBEYA HADI DAR