SAFARI YA YANGA KWENYE MICHUANO YA CAF KWA KIPINDI CHA MIAKA MITANO.

Safari ya YANGA kwenye michuano ya CAF kwa kipindi cha miaka 5 (2020/21 hadi msimu huu 2024/25) ni kama ifuatavyo.

MWAKA 2020/21.

Yanga haikushiriki kabisa michuano ya CAF kwani kwenye klabu bingwa alishiriki simba huku shirikisho walishiriki Namungo Fc, hivyo YANGA haikupata point yoyote (0×1)= 0.

MWAKA 2021/22.

Yanga walitolewa hatua za awali kabisa na Rivers united ya Nigeria hivyo kwa sababu hawakufika makundi maana yake hawakupata point yoyote (0×2)= 0.

MWAKA 2022/23.

Yanga walifika hatua ya Fainal kombe la shirikisho na kufungwa na USM Alger hivyo walikua washindi wa pili (runner-up) na walikusanya points 4 ambazo zinazidishwa kwa 3 kwa sababu ni mwaka wa 3 kimahesabu (4×3)= 12.

MWAKA 2023/24.

Yanga walifika Robo fainal ya klabu bingwa na kutolewa na Mamelod sundown hivyo kwa kufika hatua hiyo walikusanya points 3 ambazo zinazidishwa kwa 4 kwa sababu ni mwaka wa nne kimahesabu (3×4)= 12.

MWAKA 2024/25 mpaka sasa yanga wana uhakika wa points mbili (2x5=10) lakini wakifuzu kwenda Robo Fainal zitaongezeka na kua points 3 ambazo zinazidishwa kwa tano (3x5=15).

Kabla ya Kufuzu Robo Fainali points za yanga mpaka sasa ni 34 (0+0+12+12+10=34), hivyo Yanga watasalia na points 34 endapo hawatatinga hatua ya Robo Fainali.

Endapo watatinga Robo Fainal mahesabu yatakua kama ifuatvyo (0+0+12+12+15=39), ponts ambazo zitaipeleka Yanga hadi nafasi ya 5 na kuishusha waydad Casablanca .
 
Jiunge na group letu la Whtsapp 

https://chat.whatsapp.com/BXMQWuu71esFNiiOvSFsf1

MUNGU IBARIKI YANGA SC 🙏🙏



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

MAPACHA WATATU FAMILIA YA MWAIKENDA WAPATA KIPAIMARA

MVUA KUBWA KUNYESHA MIKOA 20

AINA 4 ZA WANAWAKE WASIOWEZA KUDUMISHA NDOA.

MIKOA 10 YENYE KIPATO KIKUBWA ZAIDI KWA MTU MMOJA MMOJA

BODABODA ALIPWA PIKIPIKI BAADA KUSAFIRI KWA BODA KWA SAA 10 MBEYA HADI DAR