WANAHARAKATU WANALIPWA FEDHA NYINGI KUHUJUMU SEKTA YA UTALII NCHINI

 Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimewatuhumu baadhi ya wanaharakati kulipwa fedha ili kuichafua taswira ya Tanzania kimataifa kwa lengo la kuhujumu sekta ya utalii na kupotosha dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Akizungumza na wanahabari jijini Dodoma Januari 17, 2026, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Kenani Kihongosi, amesema kuna njama zinazofanywa na watu wanaojiita wanaharakati kwa kushirikiana na baadhi ya wanasiasa kuhamasisha watalii wasije nchini, jambo ambalo ameliita ni "uangamizaji wa uchumi wa mwananchi wa kawaida."


Kihongosi amefafanua mnyororo wa thamani wa sekta ya utalii ambao unajumuisha madereva, waongoza watalii (tour guides), wamiliki wa hoteli, wafanyakazi, na wakulima wanaouza mboga na mayai kwenye mahoteli, akisema hatua yoyote ya kuichafua nchi nje ya mipaka inaenda kukata vipato vya familia hizi za Kitanzania.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

MAPACHA WATATU FAMILIA YA MWAIKENDA WAPATA KIPAIMARA

MVUA KUBWA KUNYESHA MIKOA 20

AINA 4 ZA WANAWAKE WASIOWEZA KUDUMISHA NDOA.

MIKOA 10 YENYE KIPATO KIKUBWA ZAIDI KWA MTU MMOJA MMOJA

BODABODA ALIPWA PIKIPIKI BAADA KUSAFIRI KWA BODA KWA SAA 10 MBEYA HADI DAR