RAIS SAMIA AKIPATIA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA ZAIDI YA SH. BIL 48
on
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetoa shilingi 48,469,498,473/= kwa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA) kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET),kwa ajili ya kuboresha utekelezaji wa majukumu yake ya msingi ya kutoa mafunzo, kufanya tafiti na kutoa ushauri wa kitaalam.
Kiasi hicho cha fedha kimetangazwa na Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu miradi ya maendeleo na fursa kwa vijana leo Februari 20, 2026, katika ukumbi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mtumba jijini Dodoma.
Ametaja maeneo ya kipaumbele ya utekelezaji wa mradi huo kuwa ni; ujenzi na uboreshaji wa miundombinu, kufanya mapitio ya mitaala kuendana na mahitaji ya soko la ajira, kuimarisha uhusiano na sekta binafsi, kuimarisha matumizi ya teknolojia na kuimarisha miundombinu ya TEHAMA na kuwajengea uwezo wafanyakazi.
Aidha, Prof. Sedoyeka ameelezea moja ya mafanikio ya chuo hicho kuwa ni uatamizi wa zaidi ya vijana 8600 kati yao vijana 1520 wakibuni mawazo mbalimbali ya biashara na kufanikiwa kuanzisha biashara zaidi ya 50 ambapo katika hizo kampuni 12 zilisajiliwa.
"Makampuni yaliyoanzishwa na kusajiliwa yamejikita katika maeneo ya biashara,ubunifu katika teknolojia, sanaa, uhifadhi,uhifadhi wa mazingira na maeneo mengine ambayo yametoa nafasi kwa wanafunzi wetu kujiajiri wenyewe na kuajiri vijana wenzao," amesema Prof. Sedoyeka.
Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha(IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu miradi ya maendeleo na fursa kwa vijana leo Februari 20, 2026, katika ukumbi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mtumba jijini Dodoma.
Wanahabari wakiwa katika mkutano huo.
Prof. Sedoyeka akitoka ukumbini baada ya kumaliza mkutano huku akisindikizwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO, Kelvin Kinje aliyeuongoza mkutano huo.
1. Wahiraki, Hawa ni wanawake wa jamii ya Wahiraki wa napatikana kaskazini mwa Tanzania wamezagaa mikoa ya manyara ni weupe Wana Umbo zuri wanavutia kwa Macho. 2. Warangi, Hawa ni wanawake jamii ya Warangi ni wazuri nywele zao ni asili ya waraabu weupe sura nzuri wanapatikana kondoa. 3. Wanyiramba. Hawa ni warembo Sana sura matata wanapatikana mkoa wa singida kaskazini, usipokua makini utawafananisha na wanyaturu 4. Wamasai, kabila hili wanawake wazuri sio wengi Sana lakini ukikutana na sampuli Tatu au nne hivi utauza hata boxa kuongezea mahari wamezagaa Sana Arusha 5. Wahaya, hawa nao ni jamii ya Kanda ya ziwa maumbile Yao Kuna weupe miguu Yao ya bia shape matata wamejaa Sana bukoba. 6. Wanyaturu, Hawa wanafanana na Wanyiramba wanapatikana singida hasa ikungi na manyoni weupe wanavutia 7. Wapare, Hii ni jamii ya kabila la Wapare wanapatikana moshi wilaya ya same wako vizuri usicheze kabisa na hili kabila shape nzuri. 8 .Wamakonde, ...
Image copyright BBC World Service Image caption Besigye anawania urais kwa mara ya nne Kanali (Mstaafu) Dkt Kizza Besigye Kifeefe alizaliwa mwaka 1956 katika wilaya ya Rukungiri, magharibi mwa Uganda. Besigye alifuzu kama daktari baada ya kusomea Chuo Kikuu cha Makerere, mjini Kampala. Alijiunga na chama cha Museveni cha Uganda Patriotic Movement muda mfupi baada ya kuondolewa madarakani kwa Idi Amin 1978. Mwaka 1982, alijiunga na Museveni vitani baada ya kuzuiliwa miezi miwili katika hoteli moja mjini Kampala akituhumiwa kushirikiana na waasi. Baada ya Museveni kuingia uongozini, alimteua Dkt Besigye, wakati huo akiwa na umri wa miaka 29, kuwa waziri wa nchi aliyesimamia masuala ya ndani na masuala ya siasa za taifa. Dkt Besigye alipanda cheo jeshini na kufikia cheo cha kanali. Alistaafu muda mfupi kabla ya uchaguzi mkuu wa 2001, miezi michache kabla ya kujitokeza na kutangaza kwamba angewania urais. Image copyright AFP Image caption Besigye aliwahi kukimbilia uhami...
1). Usipayuke sauti juu kwa mumeo kwa sababu yoyote . kupayuka maneno Ni ishara ya kukosa heshima. 2). Usiongee udhaifu wa mumeo kwa familia au marafiki zako. Utarudi kwako. Wewe ni mlinzi wa kila mmoja Kwa mumeo.. 3). Kamwe usitumie mitazamo na hisia kuwasiliana na mumeo, hujui jinsi mumeo atakavyoutafsiri. Wanawake wanaojitetea hawana nyumba yenye furaha. 4). Kamwe usimlinganishe mumeo na wanaume wengine, hujui maisha yao yanahusu nini. Ukimshambulia familia yake, Upendo wake kwako utapungua. 5). Usiwatendee vibaya marafiki wa mumeo kwa sababu humpendi, mtu anayepaswa kuwaondoa ni mumeo. 6). Usisahau kamwe kwamba mumeo alikuoa, si mjakazi wako au mtu mwingine yeyote. Timiza majukumu yako. 7). Kamwe usimpe mtu yeyote jukumu la kumjali mumeo, watu wanaweza kufanya kila kitu kingine lakini mumeo ni jukumu lako mwenyewe. 8. Kamwe usimlaumu mumeo akirudi nyumbani mikono mitupu. Badala yake umtie moyo. 9). Kamwe usiwe mke mharibifu, jasho la mumeo ni la t...
Image copyright AP Image caption Dkt Besigye amekamatwa akielekea makao makuu ya Tume ya Uchaguzi Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. Watu walioshuhudia wanasema amekamatwa alipokuwa akijaribu kuondoka nyumbani kwake. Amekuwa kwenye kizuizi cha nyumbani tangu Ijumaa wakati polisi walimtuhumu kupanga kujitangazia matokeo. Mtazamo wa Kizza Besigye kuhusu uchaguzi Museveni: Uchaguzi wa Uganda ulikuwa shwari Image caption Besigye alizuiliwa na polisi mara tatu wiki iliyopita Wakili wake amethibitisha habari za kukamatwa kwake. Awali kulikuwa na habari kwamba angefika makao makuu ya Tume ya Uchaguzi kuitisha matokeo rasmi ya kina ya uchaguzi wa urais. Image copyright AFP Image caption Polisi walivamia afisi za chama cha FDC Ijumaa wiki iliyopita Tume ya Uchaguzi ilimtangaza Rais Yoweri Museveni kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Alhamisi wiki iliyopita.
1. Kuzungumza na mpenzi wako kwa heshima 2. Kuhifadhi baadhi ya sehemu za mwili wako kwa ajili ya Mpenzi wako ili aone tu, usitoe Penzi kwa Kila aneomba 3. Mmbusu mpenzi wako bila sehemu yoyote 4. Kumshikilia mpenzi wako mahali anapopenda kushikwa - kiuno, mikono, mgongo, vidole nk 5. Jibu Message za mpenzi wako. Kamwe usimfanye mpenzi wako ahisi kukataliwa Kwa kutojali msg zake 6. Mpe mpenzi wako amani. Amani ni jambo muhimu Katika mahusiano 7. Kuwasiliana vizuri. Kuwa Rafiki wa kuwasiliana. Endelea kuwasiliana asubuhi, mchana na Usiku .Usiwe mgeni kihisia kwa mwenzi unayetarajia kukupa mwili wake 8. Kuvaa vizuri kwa ajili ya Mpenzi wako, kunukia vizuri, kudumisha usafi mzuri wa Mwili. 9. kuwa mtukutu, mchafu na mchafu faraghani na mpenzi wako. Inafanya urafiki uhisi kama siri kati yenu wawili 10. Kujiamini. Inamvutia mpenzi wako na kumfanya asikuache tena
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Tanzania (UWT) Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC) akitoa cheti kwa Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Dodoma, Dkt. Neema Majule ikiwa ni miongoni mwa mikoa iliyoshiriki kufanya kampeni na kutafuta kura za kishindo kwa Mgombea wa Nafasi ya Urais kwa Tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wabunge pamoja na Madiwani katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 29, 2025. Aidha, Chatanda alitoa vyeti vya Shukrani pia kwa Viongozi wa UWT kwa kila Mkoa Nchini, pamoja na Maafisa Tehama waliohakikisha kila taarifa za Uchaguzi zinawekwa kwenye mfumo mmoja na kupata takwimu sahihi kwa kile kilichofanyika katika kusaka ushindi wa kishindo kwa CCM. Hayo yamejiri Februari 14, 2026 wakati wa kikao cha Baraza Kuu la UWT kilichoketi katika ukumbi wa NEC jijini Dodoma. Dkt. Majule akipokea cheti hicho kutoa kwa Mwenyekiti wa UWT Taifa, Chatanda. Dkt. Majule akifurahia na viongozi wenzie kupata cheti hicho. IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA - 0754264203
" Tunatambua kuwa tunacheza dhidi ya klabu kubwa zaidi Afrika, klabu ya karne na hilo linahitaji heshima. Lakini kama tunataka kuwa sehemu ya historia ya soka la Afrika, si suala la kuwa na hofu ni suala la kucheza mpira. Mwisho wa siku tunakuja kucheza na kujaribu kuwashinda wapinzani wetu, huo ndio mpango wetu wa kesho. Ili ufikie kiwango cha juu lazima ucheze dhidi ya timu bora. Tunaamini kikosi chetu kina ubora, wachezaji wana kiwango na wana hamu ya kutoa kila kitu kwa ajili ya timu. Tunawaamini wachezaji wetu na tunaamini kuwa kesho tutapata matokeo tunayoyataka" Kocha mkuu Pedro Goncalves #timuyawananchi #daimambelenyumamwiko
JUMUIYA ya Umoja wa Wanawake ya Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), imetoa msaada wa vifaa tiba katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma ikiwa ni moja ya shamrashamra ya kuadhimisha miaka 49 ya kuzaliwa kwa chama hicho. Akitoa msaada huo kwa niaba ya Mwenyekiti wa UWT, Mary Chatanda, Katibu Mkuu wa UWT, Suzani Kunambi amesema kuwa vifaa hivyo vyenye thamani ya sh. mil. 20 ni maalumu kwa ajili ya Wodi za wajawazito na watoto Njiti. Ametaja vifaa hivyo vilivyopokelewa na Mganga Mfawidhi msaidizi wa hospitali hiyo, Sara Ludovick kuwa ni; vitanda, mashine za kuleta joto kwa watoto Njiti, sabuni, mafuta na khanga. Katibu Mkuu na wajumbe alioambatana nao walipata wasaa wa kuwatembelea wodi za wazazi na watoto njiti na kuwagapatia wazazi baadhi ya vifaa hivyo pamoja na vitu hivyo vingine. Kunambi ambaye aliambatana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, baadhi ya viongozi wa UWT Taifa, UWT Mkoa wa Dodoma, Wilaya ya Dodoma walipanda miti kwenye viunga vya hospitali hiyo. ...
Comments