MAREKANI YATOA TAHADHARI ZA KIUSALAMA KWA RAIA WAKE WANAISHI QATAR

Ubalozi wa Marekani mjini Doha, Qatar, umetangaza hatua ya tahadhari ya kujisitiri ndani (shelter-in-place) kwa raia wake wote, huku ukiwashauri raia wa Marekani walioko nchini humo kufanya vivyo hivyo hadi itakapotolewa taarifa nyingine.

Katika taarifa rasmi kupitia mtandao wa X, ubalozi huo ulisema: "Ubalozi wa Marekani nchini Qatar umeanzisha mpango wa kuhakikisha wafanyikazi wake wote walioko nchini humo wamebaki ndani eneo salama. Tunapendekeza Wamarekani wote wafanye hivyo hadi ilani nyingine itangazwe."

Raia wa Marekani wametakiwa kutafuta eneo salama ndani ya makazi yao au katika jengo lingine lililo salama, na kuhakikisha wanakuwa na akiba ya chakula, maji, dawa na mahitaji mengine muhimu.

Pia wamehimizwa kutoshiriki maandamano, kuwa makini na waangalifu wa mazingira yanayowazunguka, na kufuatilia taarifa kadri zinavyochipuka kupitiavyombo vya habari vya ndani.

Taarifa hiyo imeongeza: “Weka simu yako ikiwa na chaji na udumishe mawasiliano na familia na marafiki ili kuwajulisha hali yako.”

Aidha, raia wametakiwa kujisajili katika mpango wa Smart Traveler Enrollment Programme (STEP) ili wapokee taarifa za usalama kwa wakati.

Kwa huduma za dharura nchini Qatar, ubalozi umeelekeza raia kupiga nambari 999.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Wasifu wa Kizza Besigye

KILA MWANAMKE ANAPASWA KUFAHAMU HII...

MBUNGE DKT. MAJULE ATOA MSAADA WA VYAKULA, VYANDARUA 100 SHULE YA VIZIWI DODOMA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

MAMBO MADOGO YANAYOVUTIA KWA MPENZI WAKO

DKT. MAJULE AKABIDHIWA CHETI CHA SHUKRANI UWT DODOMA KUFANIKISHA USHINDI WA CCM 2025

MAJESHI YA URUSI CHINA NA IRANI YAANZA MAZOEZI YA PAMOJA DHIDI YA MAREKANI

PUNGUZA STRESS....