Mwanariadha wa Tanzania, Gabriel Gerald Geay, ameibuka mshindi wa mbio za Daegu Marathon 2026.
Mbio hizo zimefanyika tarehe 22 Februari, 2026 katika Mji wa Daegu, Korea Kusini, ambapo Geay ameongoza kwa kutumia muda wa saa 2:08:08.
Geay ameandika rekodi ya kushinda medali ya Dhahabu kwa mara ya pili mfululizo, baada ya kutwaa ushindi huo pia mwaka jana.

Comments