RAIS SAMIA AMLILIA KARDINALI PENGO

Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.

Katika kipindi chote cha utumishi wake, Kardinali Pengo alisimama imara katika kuhubiri amani, maadili na mshikamano wa kitaifa. Alikuwa sauti ya busara katika masuala ya kijamii na kimaadili, akihimiza amani, heshima na utu katika jamii yetu. Mchango wake katika malezi ya kiroho na maendeleo utaendelea kukumbukwa na kuenziwa siku zote.

Ninatoa pole kwa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Wolfgang Pisa, Maaskofu, Mapadri, Watawa, familia, ndugu, jamaa, marafiki, waumini wa Kanisa Katoliki na Watanzania wote kwa msiba huu.

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

Amina.



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Wasifu wa Kizza Besigye

KILA MWANAMKE ANAPASWA KUFAHAMU HII...

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

ASANTE GWIJI YAYA TOURE KWA KUPASUA UKWELI UKWELI KUPENDELEWA KWA MOROCCO

MAMBO MADOGO YANAYOVUTIA KWA MPENZI WAKO

DKT. MAJULE AKABIDHIWA CHETI CHA SHUKRANI UWT DODOMA KUFANIKISHA USHINDI WA CCM 2025

HATUNA HOFU KUCHEZA NA AL AHLY- KOCHA WA YANGA

UWT YATOA MSAADA WA VIFAA TIBA HOSPITALI YA RUFAA DODOMA