JOPO LA WATALAAMU KWENDA MIKOANI KUHAKIKI VIJANA WANAOTARAJIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA JKT YA KUJITOLEA


Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema timu ya wataalam kutoka Makao Makuu ya JKT iko tayari kwenda katika Mikoa yote Tanzania ili kufanya uhakiki wa vijana wanaotarajiwa kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa kujitolea.  


Brigedia Jenerali  Mabena ameyasema hayo leo tarehe 17 Februari 2026 muda mfupi baada ya kufungua Semina Elekezi kwa Maafisa waandikishaji wa vijana wa kujitolea 2026 kwa niaba ya Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele iliyofanyika katika ukumbia wa Mabele uliopo Jijini Dodoma.


Aidha, Brigedia Jenerali  Mabena ameongeza kuwa timu hiyo inayojumuisha wataalam mbalimbali ni miongoni mwa Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma ambao wamekula kiapo cha Utii na Uaminifu wapo tayari kutekeleza jukumu hilo.


Itakumbukwa Januari 20, 2026 Jeshi la Kujenga Taifa kupitia vyombo vya Habari lilitoa wito wa Vijana wote toka Tanzania Bara na Visiwani kujiunga na Mafunzo ya JKT kwa Kujitolea.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Wasifu wa Kizza Besigye

ASANTE GWIJI YAYA TOURE KWA KUPASUA UKWELI UKWELI KUPENDELEWA KWA MOROCCO

CONFIRMED HAWA NDIO WACHEZAJI WETU 12 WA KIGENI 🦾

KILA MWANAMKE ANAPASWA KUFAHAMU HII...

RAIS WA SENEGAL AWAPATIA ZAWADI NONO WACHEZAJI WALIOFANIKISHA UBINGWA WA AFCON 2025

NYOMI YA WASENEGALI WAKISHANGILIA UBINGWA WA AFCON 2025

TANZANIA YAPANDA VIWANGO VYA FIFA

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

MAMBO MADOGO YANAYOVUTIA KWA MPENZI WAKO