Maafisa kadhaa waandamizi nchini Iran wanajulikana kuuawa katika mashambulizi ya Jumamosi dhidi ya nchi hiyo.
Miongoni mwao ni:
- Ayatollah Ali Khamenei, Kiongozi Mkuu wa Iran, ambaye aliuawa Jumamosi asubuhi katika ofisi yake.
- Televisheni ya Iran imeripoti kuwa mkuu wa majeshi ya nchi hiyo, Abdolrahim Mousavi, aliuawa katika mashambulizi ya anga.
- Tehran pia imethibitisha kifo cha kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi, Jenerali Mohammad Pakpour.
- Vyombo vya habari vya serikali pia vimeripoti kuwa binti wa Khamenei, mkwe wake na mjukuu wake waliuawa katika shambulizi hilo.
- Chanzo cha kijasusi na chanzo cha kijeshi vimeiambia CBS News kuwa kwa jumla maafisa wa Iran takribani 40 waliuawa katika mashambulizi hayo.

Comments