Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete amepongeza kuteuliwa kwa Katibu Mkuu wa CCM, Dk Emmanuel Nchimbi na kwamba chama hicho kimempata mtu sahihi anayekijua chama na atakisaidia ndani na nje ya chama.
Ametoa pongezi hizo alipopata wasaa wa kuzungumza na wananchi wakati wa uzinduzi wa taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi y.a CCM ya mwaka 2025 katika Jimbo la Mchinga linaloongozwa na Mbunge Salma Kikwete ambaye ni mke wake.
Comments