UWT YAFANIKISHA IFTAR YA KUMUOMBEA DUA RAIS SAMIA

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Taifa, Mary Chatanda (kushoto) akiwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Dodoma, Pili Mmbaga wakishiriki kumuombea dua maalumu Rais Samia Suluhu Hassan wakati wa Iftar iliyoandaliwa na UWT katika msikiti wa Gaddaf jijijni Dodoma Machi 29, 2025.

Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Dkt.Alhaj Mustafa Rajabu Shaban ameipongeza Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa CCM Taifa (UWT), kwa kuwaandalia  iftar ya kumuombea dua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Msikiti wa Gaddaf jijini Dodoma.

Sheikh amesema kuwa ni haki Rais Samia kumuombea dua kwani hata yeye kwa utafiti wake amegundua kwamba ni kiongozi anayeongoza kwa kuombewa duwa za siri na za hadharani kwani anawafanyia mema watanzania jambo ambalo hata Mungu anapenda.

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi wa UWT Taifa  na wa mkoa huo wakiongozwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda,Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, viongozi na waumini wa msikiti huo wakiongozwa na sheikh huyo, Jumuiya mbalimbali za kiislamu pamoja na makundi ya watu wenye uhitaji.

Mwenyekiti wa UWT Taifa, Mary Chatanda,amewaomba Watanzania ifikapo Oktoba wakati wa Uchaguzi Mkuu wasipoteze muda kuwapigia kura ya urais wagombea wanaume wa chama chochote,  bali kura zote wampigie Dkt. Samia Suluhu Hassan wa CCM.


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) Taifa, Mary Chatanda (kushoto) akiwa na Katibu wa CCM Mkoa wa Dodoma, Pili Mmbaga pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (kulia).





Waumini wa Kiislamu wakishiriki kuomba dua hiyo.


Wakipata futari











 









IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 
MSIMAMIZI MKUU 
KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV 
0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MWABUKUSI ATOA NENO SIMBA KUSUSIA DERBY DHIDI YA YANGA

HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO

MWANAMKE ALIYEVUNJA REKODI KWA KUZAA WATOTO 69

BODI YA LIGI YAKIRI MAKOSA, WAIOMBA YANGA WAYAMALIZE

BODI YA LIGI SASA WAOMBA HEKIMA NA BUSARA ITUMIKE DERBY YA YANGA, SIMBA