Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.Samia Suluhu Hassan ameupongeza mkoa wa Pwani kwa kasi kubwa ya maendeleo ya viwanda ambapo idadi imeongezeka kutoka viwanda 1,587 hadi viwanda 1,631 kwa mwaka huu.
Amesema kuwa ongezeko hilo sawa na ongezeko la viwanda 244 ndani ya miaka minne au viwanda 61 kila mwaka.
Amefafanua kuwa viwanda vya kati 81 vimejengwa ambapo sasa vimefikia 161 sawa na viwanda 26 kila mwaka na kwamba vimetoa ajira za moja kwa moja 21,146 na zisizokuwa za moja kwa moja ajira 60,000.
Amepotoa pongezi hizo katika mkutano wa kampeni za CCM kwenye viwanja vya Sabasaba Kibaha mkoani Pwani Septemba 28,2025.
“Hapa sijavitaja viwanda vidogo ambavyo vimewanufaisha Watanzania wengi kwa bidhaa zinazozalishwa nchini.Uwekezaji uliofanyika umewezesha nchi yetu kupiga hatua kujitegemea kimapato na bidhaa.
“Kwa mfano ndani ya Mkoa wa Pwani kuna uzalishaji mkubwa unaofanya nchi ijitegemee kwenye bidhaa muhimu.”Sasa tunajitegemea kwenye uzalishaji vioo lakini marumaru, saruji, mabati ya rangi vyote vinazalishwa ndani ya nchi."
Pia Dk. Samia amesema kutokana na kasi kubwa ya ukuaji viwanda serikali imeamua kujenga vituo vya kupoza umeme eneo la Msufini Mkuranga kwa gharama ya sh. bilioni 388.3.
“Kituo kingine kitajengwa Zegereni Kibaha kwa gharama ya sh. bilioni 54.7 na Zinga Bagamoyo kwa sh. bilioni 120.Umeme huo utakuwa wenye uhakika kuufanya mkoa huo kutokumbwa na upungufu wa umeme, hivyo viwanda vitazalisha muda wote.
๐ฅ๐๐๐ฆ ๐๐๐ง. ๐ฆ๐๐ ๐๐ ๐๐ ๐๐ช๐๐๐๐ก๐๐๐ ๐ช๐๐ก๐๐ช๐๐๐ ๐ ๐ข๐ฌ๐ข ๐ช๐ ๐จ๐๐๐ฆ๐๐๐ ๐ก๐ ๐๐จ๐๐๐๐ ๐๐ก๐ ๐ผ๐ข๐๐๐ก๐๐ฏ๐ ๐๐๐ฉ๐๐๐ช ๐๐ ๐ช๐ช ๐ข๐จ๐ฉ๐๐๐๐ช ๐ฌ๐ ๐พ๐พ๐, ๐ฟ๐ ๐ฉ. ๐ฝ๐๐จ๐๐๐ง๐ช ๐ผ๐ก๐ก๐ฎ "Kwa muda mrefu katika historia ya siasa Duniani kote, nafasi ya mwanamke imekuwa nafasi ya pili kanakwamba utu wake ni nusu..duniani kote ajenda ya kuweka usawa kwa wanaume na wanawake imekuwa mfupa mgumu.." "..CCM kwasababu ya msimamo wetu wa kifalsafa na kiitikadi, usawa wa wanaume na wanawake si suala la hiari ni saula la lazima.." "..katika uongozi wako Rais Dkt. Samia...kitakwimu katika kipindi ulichoingia kama Mkuu wa nchi na Mwenyekiti wa chama (CCM) , kitakwimu angalieni maamuzi, sera, miradi na namna utekelezaji wake ulivyoinua hali za akina Mama.." Dkt. Bashiru ameyasema hayo leo tarehe 9 Septemba 2025 wakati akizungumza na maelfu ya Wananchi wa Singida Mjini waliojitokeza katika uwanja wa Bombadia kumlaki na kumsikiliza Mgombea...
Comments