UJENZI MRADI WA GESI ASILIA MBIONI KUANZA LINDI


 Na Richard Mwaikenda, Lindi

MGOMBEA Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amewakikishia Wananchi wa Mkoa wa Lindi kwamba mradi mkubwa wa gesi asilia aina ya NLG wenye thamani ya sh. bil. 40 uko mbioni kuanza.


Ametoa uhakika huo alipokuwa akihutubia katika mkutano wa Kampeni za CCM kwenye Uwanja wa Ilulu Lindi Mjini Septemba 25,2025.


Amesema kuwa wapo katika hatua za Mwisho za makubaliano na mwekezaji wa mradi huo ili kila upande ujue utafaidikaje na mradi.


"Mradi wa bil. 40 ni mkubwa, Mwekezaji lazima  awe na uhakika, nasi pia tuwe na uhakika tutapata nini kupitia rasilimali yetu  hiyo. Tupo hatua za mwisho za makubaliano. Mradi upo na utaanza, ndiyo maana Chuo kinaendelea kujengwa ili vijana wetu wapate ajira, " ametoa uhakika huo Dkt. Samia.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MBINU ZITAKAZOKUFANYA USIISHIWE PESA

DKT. MIGIRO AKIWASHA KAMPENI ZA DKT. SAMIA MAKAMBAKO

LEO NI LEO KAMPENI ZA DKT. SAMIA SONGWE

NENO KUNTU LA UMMY MWALIMU ALILOLITOA BAADA YA KUTEMWA KUGOMBEA UBUNGE

WAGOMBEA WALIOENGULIWA CCM LICHA YA KUONGOZA KURA ZA MAONI

CHONGOLO AMKUMBUKA DKT. ASHA-ROSE MIGIRO-