KAMPENI ZA DKT SAMIA KURINDIMA BUKOBA MJINI LEO

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, leo anafanya mkutano mkubwa wa kampeni mjini Bukoba, mkoani Kagera.


‎Dkt. Samia ambaye yupo kwenye muendelezo wa kampeni za Uchaguzi Mkuu, Jana amefanya katika Wilaya za Muleba, Misenyi na Karagwe ambapo ameeleza miradi mbalimbali iliyotekelezwa wakati wa uongozi wake wa miaka minne na kutoa ahadi lukuki atakazozitekeleza endapo wananchi watampatia ridhaa ya kuongoza tena Nchi kwa kumchagua katika Uchaguzi Mkuu Oktoba 29.


‎Baadhi ahadi alizozitoa katika mikutano hiyo ni; ujenzi wa Uwanja wa Ndege mkubwa wa kisasa wa Kimataifa, kujenga kongani za viwanda vikiwemo vya kuongeza thamani ya mazao ya samaki kuinua zao la alovera,  zao la kahawa, kununua boti za  uvuvi zitakazotolewa mkopo kwa wavuvi.


‎Pia, atahakikisha anakamilisha miradi mbalimbali ya maendeleo ya maji, elimu, umeme, barabara pamoja na kujenga miradi mingine mipya.



 IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

KIGOGO WA CHADEMA AHAMIA CCM

DKT.NCHIMBI ATUA RASMI SONGEA KUSAKA KURA ZA CCM

DKT. SAMIA AAHIDI KUJENGA CHUO CHA UHASIBU SONGEA

IJUE HISTORIA YA PACOME ZOUZOUA