MWANZA WAAHIDI KUMPATIA DKT. SAMIA USHINDI WA KISHINDO


.Na Richard Mwaikenda, Buhongwa, MWANZA

 Mkoa wa Mwanza wameahidi kumpatia ushindi wa kishindo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika majimbo yote 9 ya Uchaguzi.


Ahadi hiyo imetolewa kwa niaba ya wananchi  na Mwenyekiti wa CCM  wa Mkoa huo, Michael Nasanja alipokuwa akitoa salamu za Mkoa  akimkaribisha DKT. Samia mkoani humo katika mkutano wa Kampeni katika Kata ya Buhongwa, Nyamagana Oktoba 7, 2925.


Amesema kuwa wananchi watampatia ushindi huo kutokana na kuuletea Mkoa huo maendeleo makubwa yanayoonekana na kila mtu.


Serikali inayoongozwa na Rais, DKT. Samia imepeleka mkoani humo zaidi ya sh. 5 za ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo miundombinu ya barabara, afya, elimu, maji, Kilimo, nishati na mawasiliano.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

KIGOGO WA CHADEMA AHAMIA CCM

MBINU ZITAKAZOKUFANYA USIISHIWE PESA

DKT.NCHIMBI ATUA RASMI SONGEA KUSAKA KURA ZA CCM