Na Richard Mwaikenda, Rukwa
Ametoa kauli hiyo alipopewa wasaa wa kutoa salamu katika mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye viwanja vya Kizwite Sumbawanga Mjini mkoani Rukwa Oktoba 19, 2025.
"Leo CHADEMA imegeuka kuwa NGo's inapewa fedha na wanaharakati walioko Nje ya Nchi, wanachangiwa kwenye mitandao, yaani Chama kiko Tanzania lakini kinaendeshwa kwa 'remote control'na watu walio nje wenye fedha zao. na wakileta pambano nitakuja na orodha ya majina yao,"amesema Wenje.
"CCM hoyee, kwa hiyo mimi kwa maoni yangu na dhamira yangu naamini nimechagua njia iliyo sahihi. Naamini Watanzania tutakuwa salama na tutakuwa tumechagua njia sahihi Oktoba 29 tukimpigia Dkt Samia kura, wabunge wa CCM na Madiwani wa CCM."
Jana Oktoba 18, 2025, Wenje akiwa katika mkutano wa Kampeni Mpanda Mjini, mkoani Katavi alitaja baadhi ya nchi za nje zinazofadhili kuwa ni; Marekani, Norwey, Uingereza na Kenya.
Comments