Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb) amewashukuru OWM-Kazi, Ajira na Mahusiano kwa kumtambua kama aliyechangia mabadiliko katika sera ya Kinga ya Jamii.
Mh.Kikwete amesema kuwa nishani hiyo ataipeleke kwa Mh. Samia Suluhu Hassan, Rais wa JMT kwa kumpa nafasi ya kutumika katika nchi hii chini ya Uongozi wake.
Amemshukuru Mh.Rais toka kwenye sakafu ya Moyo wake kwa kumteua na kumuamini siku zote. Ameendelea kuahidi kuwa atatumika kwa manufaa na ujenzi wa nchi.

Comments