Muonekano wa eneo la Mradi wa ujenzi wa Matanki ya kupokea mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam, Kigamboni Jijini Dar es Salaam. Ujenzi wa Matanki hayo utasaidia kupunguza au kuondoa kabisa uhaba wa mafuta Nchini, kuimarisha usalama wa nishati hiyo, kupunguza muda wa meli kusubiri nangani kutoka wastani wa siku 22 hadi siku 7, kupunguza muda wa kushusha shehena ya mafuta kutoka siku 7 hadi siku 1, kuongeza mapato ya Taifa kupitia makusanyo ya kodi na tozo mbalimbali zitakazo kusanywa na Mamlaka husika pamoja na kutoa ajira kwa Watanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa matanki hayo.



Comments