Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Ndg, Mussa Mohammed Makame amesema Watanzania hawapaswi kuwa na hofu kwani mpaka sasa nchi haijapata athari yoyote.
Ameyasema hayo jijini Dodoma leo Machi 11, 2026 alipokuwa akijibu swali la mwandishi kuhusu hali ya upatikanaji wa mafuta kufuatia vurugu zinazoendelea katika baadhi ya maeneo duniani katika mkutano wa kuelezea mafanikio ya TPDC katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.
Amesema kauli hiyo inaenda sambamba na ufafanuzi uliotolewa hivi karibuni na Waziri wa Nishati, Deogratias Ndejembi, aliyewahakikishia wananchi kuwa hali ya upatikanaji wa mafuta nchini iko salama.
Kwa mfano, mafuta yanayotumika mwezi Machi yaliagizwa mwezi Januari, na yatakayotumika Aprili yaliagizwa Februari.





Comments