ZAIDI YA WATU 200 WAFARIKI BAADA MGODI KUPOROMOKA DR CONGO

Serikali ya Jamhuri ya demokrasia ya Congo imesema zaidi ya watu 200 wamefariki, wakiwemo watoto 70, baada ya maporomoko ya ardhi mashariki mwa nchi hiyo.

Maporomoko hayo yalitokea katika eneo la Rubaya, ambalo ndilo chanzo kikubwa cha madini ya coltan nchini humo.

Tukio hilo lilitokea Jumanne baada ya mvua kubwa kunyesha katika eneo hilo ambalo linadhibitiwa na waasi.

Katika taarifa ya wizara ya madini ililaumu kundi la waasi la M23, ikisema wanaruhusu uchimbaji wa madini kinyume cha sheria bila kufuata viwango vya usalama.

Kundi la M23 bado halijatoa kauli yoyote kuhusu tukio hilo. Hata hivyo, chanzo kimoja kutoka Rubaya kiliiambia BBC kuwa kuporomoka huko kwa mgodi kulisababishwa na mashambulizi kutoka kwa majeshi ya serikali, na kwamba watu sita tu ndio waliokufa. Hata hivyo serikali bado haijajibu madai hayo.

Migodi ya Rubaya inaaminika kuwa na takribani asilimia 15 ya akiba ya coltan duniani, na karibu nusu ya akiba yote ya madini hayo nchini DR Congo.

Tangu mwaka 2024, waasi wa M23 wamekuwa wakidhibiti eneo la Rubaya, lililoko takribani kilomita 70 magharibi mwa mji wa Goma, mji mkuu wa jimbo la Kivu kaskazini.

Mamlaka zilisema juhudi za uokoaji baada ya maporomoko ya Jumanne zilikwama kutokana na hali hatari katika eneo hilo. Serikali pia iliilaumu kundi la waasi kwa kuweka vikwazo kwa raia, jambo lililofanya shughuli za uokoaji kuwa ngumu.

Wizara ya madini iliongeza kuwa kukosekana kwa usimamizi rasmi katika mgodi huo kumewaacha wachimbaji bila ulinzi wa msingi wa usalama kazini


 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

Wasifu wa Kizza Besigye

Kizza Besigye ‘akamatwa’ tena Uganda

KILA MWANAMKE ANAPASWA KUFAHAMU HII...

IRAN YAMTANGAZA AYATOLLAH MPYA

MBUNGE DKT. MAJULE ATOA MSAADA WA VYAKULA, VYANDARUA 100 SHULE YA VIZIWI DODOMA

MAMBO MADOGO YANAYOVUTIA KWA MPENZI WAKO

DKT. MAJULE AKABIDHIWA CHETI CHA SHUKRANI UWT DODOMA KUFANIKISHA USHINDI WA CCM 2025

MATUKIO RAIS, AMIRI JESHI MKUU DKT. SAMIA AKIZINDUA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA (MMUT)

WANAOTAZAMWA KUMRITHI AYATOLLAH ALLY KHAMENEI.