MONGELLA: CCM ITAWEKEZA KATIKA MIRADI YENYE TIJA


 


 

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesisitiza kuendelea kuwekeza katika miradi mbalimbali ya maendeleo kama vile barabara, elimu, na maji, ili kuhakikisha wananchi wengi wanapata maendeleo kupitia juhudi za serikali. Akizungumza katika Halmashauri ya Msalala, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John Mongela, alisema kuwa hatua hizi tayari zimeleta matunda, hasa kupitia huduma bora za afya ambazo zimeboresha maisha ya wananchi.


Mongela aliongeza kuwa serikali imekamilisha mchakato wa kumpata mkandarasi wa mradi wa barabara kutoka wilaya ya Kahama kuelekea Kakola, barabara ya kilometa 73 inayounganisha mkoa wa Geita, ambayo inatarajiwa kuimarisha uchumi wa mikoa hiyo miwili.


Mkuu wa wilaya ya Kahama, Mboni Mhita, alisema zaidi ya shilingi bilioni 100 zitatumika katika mradi huo wa barabara, ambazo ni sehemu ya maono ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

CPA MAKALLA 'KUUTEKA' MKOA WA ARUSHA

DEMU KAMA ANAFANYA KAZI HIZI KUWA MAKINI NAE.

ASKOFU CHANDE AISHUKURU SERIKALI KULIPATIA USAJILI WA KUDUMU KANISA LA KARMELI

"WANAUME WAPO GEREZANI, KABURINI"

JENGENI UWANJA WA MICHEZO WA KISASA NJOMBE-MWANYIKA

KAMATI YA UWT KUTOA MSAADA WA KISHERIA NCHINI