Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati), akimsikiliza Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Godfrey Kasekenya (Mb) (kulia) kuhusu maendeleo ya ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma, ambao unatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika mwezi Septemba mwaka huu, hatua inayotarajiwa kuimarisha usafiri wa anga na kulipa hadhi zaidi jiji la Dodoma ambalo ni Makao Makuu ya nchi. Wengine katika picha ni Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Balozi Mhandisi Aisha Amour (wa pili kulia) Na Benny Mwaipaja, Dodoma Serikali imesema kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma unatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika ndani ya mwezi Septemba mwaka huu, hatua inayotarajiwa kuimarisha usafiri wa anga na kulipa hadhi zaidi jiji la Dodoma ambalo ni Makao Makuu ya nchi. Akizungumza wakati alipotembelea na kuona maendeleo ya mradi huo, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), alisema uje...
Comments