RAIS SAMIA AAGIZA SGR KWENDA ARUSHA


 ARUSHA; RAIS Samia Suluhu Hassani ameagiza uanze mchakato wa kujenga Reli ya Kisasa (SGR) kwenda mkoani Arusha.

-

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa alisema hayo alipozungumza na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda jijini Arusha juzi.

-

“Tuna mpango mkubwa sana kwa Arusha kwa maana maelekezo mahsusi ya Rais kuanza ujenzi wa SGR kuja hapa Arusha na itaambaa ambaa kwenda hadi Musoma,’’ alisema Kadogosa.

-

Alisema ujenzi wa reli hiyo ilikuwa ni matamanio ya Baba wa Taifa, Julius Nyerere na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

-

“Walisukuma hadi mahali walipofikia lakini ni matamanio ya Baba wa Taifa kuona kwamba tunaunganisha kutoka Tanga, Kaskazini itumie Bandari ya Tanga ifike Musoma ivuke kwenda Jinja,” alisema Kadogosa.

-

Imeandaliwa na Mwandishi Wetu

Soma zaidi//habarileo.co.tz

#HabarileoUPDATES

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MWABUKUSI ATOA NENO SIMBA KUSUSIA DERBY DHIDI YA YANGA

HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO

MWANAMKE ALIYEVUNJA REKODI KWA KUZAA WATOTO 69

BODI YA LIGI YAKIRI MAKOSA, WAIOMBA YANGA WAYAMALIZE

BODI YA LIGI SASA WAOMBA HEKIMA NA BUSARA ITUMIKE DERBY YA YANGA, SIMBA