ARUSHA; RAIS Samia Suluhu Hassani ameagiza uanze mchakato wa kujenga Reli ya Kisasa (SGR) kwenda mkoani Arusha.
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC), Masanja Kadogosa alisema hayo alipozungumza na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda jijini Arusha juzi.
-
“Tuna mpango mkubwa sana kwa Arusha kwa maana maelekezo mahsusi ya Rais kuanza ujenzi wa SGR kuja hapa Arusha na itaambaa ambaa kwenda hadi Musoma,’’ alisema Kadogosa.
-
Alisema ujenzi wa reli hiyo ilikuwa ni matamanio ya Baba wa Taifa, Julius Nyerere na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.
-
“Walisukuma hadi mahali walipofikia lakini ni matamanio ya Baba wa Taifa kuona kwamba tunaunganisha kutoka Tanga, Kaskazini itumie Bandari ya Tanga ifike Musoma ivuke kwenda Jinja,” alisema Kadogosa.
-
Imeandaliwa na Mwandishi Wetu
Soma zaidi//habarileo.co.tz
#HabarileoUPDATES
Comments