WANAFUNZI KUACHA KUTEMBEA KILOMITA KUMI KWENDA MASOMONI: WANAKIJIJI WAAMUA KUJENGA SEKONDARI YAO

 

Kijiji cha Kataryo ni moja ya vijiji vitatu vya Kata ya Tegeruka. Vijiji vingine ni vya Mayani na Tegeruka.


*Sababu zinazohamasisha ujenzi wa sekondari ya Kijiji cha Kataryo:*


(a) Kijiji cha Kataryo kimeshiriki kujenga sekondari za Mugango (Kata jirani ya Mugango), na Tegeruka (Kata ya Tegeruka). Sekondari hizi mbili ziko mbali na Kijiji cha Kataryo kwa umbali wa kilomita kumi (Tegeruka Sekondari), na kumi na tano (Mugango Sekondari)


(b) Mfumo mpya elimu ambao unamtaka kila kijana wa Tanzania kupata elimu ya Kidato cha Nne.


*Harambee ya Mbunge wa Jimbo ya ujenzi wa Kataryo Sekondari:*


Jana, Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo aliendesha Harambee ya kupata fedha na vifaa vya ujenzi wa Kataryo Sekondari. Matokeo yake ni:


(a) Mifuko ya Saruji

*Wanakijiji: Saruji Mifuko 171

*Mbunge wa Jimbo: Saruji Mifuko 200


(b) Michango mingine

*Wanakijiji: Nondo 32

*Wanakijiji: Mchanga tripu moja

*Wanakijiji: Tsh 150,000

*Michango ya fedha kutoka kila kaya itaanza kukusanywa hivi karibuni


KARIBUNI TUCHANGIE UJENZI WA SEKONDARI YA KIJIJI CHA KATARYO


Picha zilizoambatanishwa hapa ni za kutoka kwenye tukio la Harambee ya Kijijini Kataryo, Kata ya Tegeruka 


Ofisi ya Mbunge 

Jimbo la Musoma Vijijini 

www.musomavijijini.or.tz 


P. O. Box 6

Musoma 


Tarehe:

Alhamisi, 27 March 2025

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MWABUKUSI ATOA NENO SIMBA KUSUSIA DERBY DHIDI YA YANGA

SERIKALI YALIKUBALI OMBI LA DIAMOND

HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO

MWANAMKE ALIYEVUNJA REKODI KWA KUZAA WATOTO 69

ARAJIGA AULA KOMBE LA DUNIA

BODI YA LIGI YAKIRI MAKOSA, WAIOMBA YANGA WAYAMALIZE