WMA WAPONGEZWA KUANDAA FUTARI MAALUMU YA KUOMBEA DUA JENGO LAO JIPYA DODOMA

Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Coletha Kilawe akizungumza wakati wa hafla ya Iftar maalumu ya kuliombea dua/sala jengo jipya la Wakala wa Vipimo 9WMA) eneo la Medeli jijini Dodoma Machi 28, 2025.

Akizungumza katika hafla hiyo, Kilawe ambaye ni Afisa  Rasilimali Watu wa mkoa huo, amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa serikali anayoiongoza kutoa fedha za ujenzi wa jengo hilo la kisasa uliogharimu zaidi ya sh. bil. 6, lakini pia hakusita kuupongeza uongozi wa WMA kwa kuandaa tukio hilo jema la kuandaa hafla ya iftar maalumu ya kuliombea dua jengo hilo.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na baadhi ya viongozi wa dini, siasa, viongozi na watumishi wa WMA pamoja na majirani.


Baadhi ya viongozi walioalikwa wakipata futari.


Baadhi ya waalikwa wakijipatia mlo huo.



Mjumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Vipimo (WMA), CPA. Swalehe Chondoma akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa bodi hiyo.
John Maliga wa EAGT Baraza la CPCT.
Askofu Anthony Nyashimba wa Kanisa la Baptist na Mwenyekiti wa Umoaja wa Makanisa ya Kikristo Mkoa wa Dodoma akizungumza wakati wa sala ya kuliombea  jengo jipya la WMA.
Sheikh Ahmad Said Msemaji wa Sheikh wa Mkoa wa Dodoma akizungumza wakati wa kuomba dua.
Mkurugenzi wa Biashara wa WMA, Karim Mkorehe akizungumza kabla ya kumkaribisha CPA. Chondoma.




 

IMEANDALIWA NA RICHARD MWAIKENDA 
MSIMAMIZI MKUU 
KAMANDA WA MATUKIO ONLINE TV
 0754264203

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MWABUKUSI ATOA NENO SIMBA KUSUSIA DERBY DHIDI YA YANGA

HOSPITALI YA MUHIMBILI YAANZISHA HUDUMA YA KISASA YA KUZIBA MAPENGO

MWANAMKE ALIYEVUNJA REKODI KWA KUZAA WATOTO 69

BODI YA LIGI YAKIRI MAKOSA, WAIOMBA YANGA WAYAMALIZE

BODI YA LIGI SASA WAOMBA HEKIMA NA BUSARA ITUMIKE DERBY YA YANGA, SIMBA