RAIS SAMIA ATOA SALAMU ZA POLE KWA KIFO CHA MKURUGENZI MTENDAJI WA TANESCO

 SALAMU ZA RAMBIRAMBI 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  amemtumia salamu za rambirambi Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.  Dkt. Doto Biteko kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika La  Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Gassima Nyamo-Hanga pamoja na dereva  wake Muhajir Mohamed Haule.  

Marehemu Nyamo-Hanga na dereva wake wamefariki usiku wa kuamkia leo tarehe  13 Aprili, 2025 katika ajali ya gari iliyotokea katika Wilaya ya Bunda, Mkoani Mara.  

Rais Dkt. Samia anawapa pole Wizara ya Nishati, TANESCO, familia, ndugu, jamaa  na marafiki wa marehemu Nyamo-Hanga na Haule. 

Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu Nyamo-Hanga na Haule mahala pema  peponi, Amina. 

Sharifa B. Nyanga 

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

BREAKING NEWS | MKURUGENZI MTENDAJI WA TANESCO AFARIKI DUNIA

SHEREHE ZA DKT. CHANDE KUSIMIKWA UASKOFU MKUU KANISA LA KARMELI ZAFANA

#MAKINIKIA: HEKAYA FUPI YA MJI WA KIHISTORIA WA MOSHI MKOANI KILIMANJARO

HUU NDIO UKWELI ULIVYO RAFIKI YANGU

RATIBA KAMILI YA HARUSI YA DIAMOND, ZUCHU

ZIJUE TABIA 9 ZA WANAWAKE HAWA....

TANZANIA NI MIONGONI MWA NCHI 10 ZINAZOONGOZA KWA MAZAO YA KILIMO AFRIKA

ASKOFU CHANDE ATOA MSAADA WA MAZIWA, AWAOMBEA WATOTO NJITI