TUME YA MADINI KUENDELEA KUWASAIDIA WASAMBAZAJI NA WAUZAJI BARUTI

 Tume ya Madini imesema itaendelea kutoa ushirikiano na kuwasaidia wasambazaji na wauzaji wa baruti nchini ili wafanye shughuli zao kwa mujibu wa Sheria na kanuni za baruti zilizopo.

Mkaguzi Mkuu wa Migodi Mhandisi Hamisi Kamando amesema hayo ,Jijini Dodoma wakati akifungua kikao kazi kilichowakutanisha wadau wa baruti, pamoja na Wakaguzi wa Migodi na Baruti Nchini.

Mhandisi Kamando amesema kutokana na ongezeko la shughuli za uchimbaji wa madini kumepelekea kupanuka kwa biashara ya baruti hapa nchini.

“Ongezeko la uhitaji wa matumizi ya baruti hapa nchini imepelekea uwepo wa changamoto kadhaa katika usimamizi wake,hivyo watumishi wa Idara ya Ukaguzi wa Migodi na Mazingira kutoka Tume ya madini wataendelea na udhibiti katika maeneo yao ili kuepusha madhara,amesema.

Ametoa wito kwa wadau wa baruti nchini kujiunga katika Chama Cha Wauza Baruti Tanzania (TEDA), ili Serikali iweze kuwasaidia kwa pamoja.

Mdau wa Baruti kutoka Mkoa wa Geita Mhandisi Ramadhani Kamaka ameeleza kunufaishwa na kikao hicho na kuiomba Serikali kutoa elimu zaidi kwa mamlaka ambazo zinahusika katika usimamizi wa baruti nchini.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MWANAMKE ALIYEVUNJA REKODI KWA KUZAA WATOTO 69

BODI YA LIGI YAKIRI MAKOSA, WAIOMBA YANGA WAYAMALIZE

#MAKINIKIA: HEKAYA FUPI YA MJI WA KIHISTORIA WA MOSHI MKOANI KILIMANJARO

HUU NDIO UKWELI ULIVYO RAFIKI YANGU

BODI YA LIGI SASA WAOMBA HEKIMA NA BUSARA ITUMIKE DERBY YA YANGA, SIMBA

RATIBA KAMILI YA HARUSI YA DIAMOND, ZUCHU

TANZANIA NI MIONGONI MWA NCHI 10 ZINAZOONGOZA KWA MAZAO YA KILIMO AFRIKA

ZIJUE TABIA 9 ZA WANAWAKE HAWA....