HUYU NDIYE MOKAILA MKUFUNZI MPYA WA MAFUNZO WA MAZOEZI YANGA

π—§π—¦π—›π—˜π—£π—›π—”π—‘π—š π— π—’π—žπ—”π—œπ—Ÿπ—”

 Ni mkufunzi maarufu wa mazoezi ya mwili kutoka Botswana,Anayejulikana kwa jina la utani "Chyna".Yeye ni mmiliki wa kituo cha mazoezi kinachoitwa ULTIMATE FITNESS kilichoanzishwa mwaka 2013.

Kituo hiki kinatoa huduma mbalimbali kama vile mazoezi ya afya,Mafunzo ya kibinafsi na ya vikundi,Aerobics, Uimarishaji wa michezo, na saikolojia ya michezo.Pia anaendesha chapa yake binafsi ya mazoezi iitwayo *CMFit*, ambayo ina programu mbalimbali za mazoezi na mipango ya lishe.

01; Mokaila ana sifa za kitaaluma kutoka Australia, Marekani (National Federation of Professional Trainers), na Uholanzi (World Football Academy).Mbali na kazi yake ya mazoezi,Amekuwa mkufunzi wa mazoezi ya mwili kwa klabu kubwa ya soka nchini Botswana, *Township Rollers*, tangu mwaka 2014.

Pia, ameteuliwa kuwa mkufunzi wa mazoezi ya mwili kwa timu ya taifa ya wanaume ya Botswana, "The Zebras", wakati wa maandalizi ya mechi za kufuzu Kombe la Dunia la FIFA 2026.

02;Wakati wa janga la COVID-19, Mokaila alianzisha programu ya CMFit Virtual ambayo ilimuwezesha kuwafikia wateja wa kimataifa kutoka nchi kama Kanada, Austria, Italia, Zimbabwe.

Mpango huu ulisaidia watu wengi kubaki na afya nzuri wakati wa vizuizi vya janga hilo. 

VILABU AMBAVYO AMEPITA NI PAMOJA NA;

¤AMAZULU "SOUTH AFRICA"
¤HOROYA "GUINEA"
¤TOWNSHIP ROLLERS "BOTSWANA "
¤ALAHLI SC

Welcome Young Africans Sports Club



 

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

DUNIA NI KATILI SANA KWA MWANAUME MASIKINI

MWANAUME USIPITWE NA HILI, INASIKITISHA...?!!!

USAJILI ULIVYO HADI SASA....

HUYU NDIYE MWANAMKE WA KUOA

RAIS SAMIA AYATAKA MASHINDANO YA MISS WORLD 2027

MAMBO 7 MUHIMU YA KUYAEPUKA BAADA YA KUACHANA...